Hili
ni eneo la Kituo cha Daladala cha Ubungo jijini Dar, biashara
ndogondogo zikiwemo za viatu zinafanyika wakati huo huo waenda kwa miguu
nao wakipita eneo hilohiolo.
...Wengine wanauza samaki katika eneo ambalo kiafya si sahihi.
Nguo
za ndani zikiuzwa katika eneo hilo. Jambo ambalo husababisha msongamano
katika eneo hili na wakati mwingine kuleteleza ajali zisizo za lazima.
...Suluali zikiwa zimetundikwa pembezoni mwa barabara.
Bila kujali vumbi katika eneo hili, wauzaji wameanika T-Shirt zao na kuendelea kuuza.
....Wengine nao wanauza Urembo pamoja na vifaa vya simu.
Hii
kali sana hawa Jamaa wanauza DVD kwa Tsh 500 hadi 1,000 bei ya juu.
Swali linakuja hapa kuna kazi za nje na ndani ya Tanzania, Je Haki
miliki Mpo? na watu wa mapato hili mnalionaje?
...Wauza Redio nao wapo.
Huu
ni uzibe wa barabara kuu, ambapo pembezoni mwake waenda kwa miguu
hupita wakati huo biashara ya nguo ikiendelea kuchukua nafasi.
Katika eneo hili la Ubungo sio pembezoni mwa barabara pekee lakini hadi mabondeni biashara zinaendelea.
Hawa nao wapo wanauza Vioo vya kujitazamia pamoja na vifaa vya kuegeshea nguo.
Mikanda na Boksa navyo vinauzwa katika eneo hili.
Miwani ya wakubwa na watoto nayo ipo kwa bei chee.
Bukta nazo zinauzwa eneo hili.
Hii ndiyo hali Halisi ya eneo kutoka Ubungo Darajani karibia na mitambo ya Gesi hadi eneo la kituo cha magari ya kwenda Mwenge.
Hili ni eneo la Ubungo ambapo Kumekuwa na kero kubwa ya wafanyabishara wadogo wadogo kuweka biashara zao za kila aina pembezoni mwa njia za wapita kwa miguu jambo ambalo linasababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo.
Licha ya usumbufu huo na kero hiyo, eneo hilo kutokana na msongamano wa watu wengi sana, limekuwa ndio maskani kwa vibaka ambao hujipatia kipato chao bila hata ya jasho kwa kujichanganya humo kama raia wa kawaida na kutekeleza jukumu lao la wizi.
Wakizungumza na mtandao huu, watumiaji wa barabara hiyo wamelilalamikia Jiji na Manispaa husika kwa kushindwa kuwatafutia eneo husika wafanyabiashara hao. Kutokana na uzembe huo mkubwa wakutowazuia, nao wameamua kuendelea kuleta kero.
Je Halmashauri ya Jiji hamlioni hili? Je
Manispaa husikia nanyie hamlioni hili? Au hili ni eneo halali
limepitishwa kwa ajili ya kufanya biashara hizi?
"Eneo hili kwa kweli linatia Aibu sana kwa sababu hapa ndipo Lango kuu la kuingia jijini na mara watu wanapoingia wanakutana na kero hii ambayo mimi binafsi naita ni uchafu, nasikitika sana kuona Jiji na Halmashari husika wameshindwa kabisa kudhibiti na kuwatafutia eneo husika hii ni aibu" .
"Eneo hili kwa kweli linatia Aibu sana kwa sababu hapa ndipo Lango kuu la kuingia jijini na mara watu wanapoingia wanakutana na kero hii ambayo mimi binafsi naita ni uchafu, nasikitika sana kuona Jiji na Halmashari husika wameshindwa kabisa kudhibiti na kuwatafutia eneo husika hii ni aibu" .
Alizungumza mmoja wa watumiaji wa barabara hiyo ambaye hupita mara kwa mara.
PICHA NA DAR ES SALAAM YETU
0 comments:
Post a Comment