Mgeni
rasmi katika Sherehe za maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu Waziri
Mkuu Mh. Mizengo Pinda akiwasili katika viwanja vya Mnazi Mmoja na
kusalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa
Mataifa nchini (UNDP) Bw. Phillippe Poinsot.
Pichani
Juu na Chini ni maandamano ya kuadhimisha siku ya Haki za Binadamu
yaliyohusisha Taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali,
Wanafunzi wa Shule za Sekondari na Wanaharakati wa Haki za Binadamu
yakiwasili katika Viwanja vya Mnazi Mmoja na kupokelewa na Mh. Waziri
mkuu Mizengo Pinda (hayupo pichani).
Meza
Kuu ikipokea maandamano ya Wanafunzi na Taasisi mbalimbali za
Kiserikali na zisizo za Kiserikali wakati sherehe za maadhimisho ya Siku
ya Haki za Binadamu zilizofanyika jijini Dar leo.











