Na.Mwandishi wetu Dodoma.
Mbunge wa Ilala Musa Azan Zungu leo amekanusha kukamatwa na Rushwa na takukuru kwenye mkutano mkuu wa jumuia ya wazazi uliofanyika juzi. Zungu amesema kuwa magazeti yamekaririwa kupotosha ukweli kuwa yeye Zungu alikuwa amekamatwa na Rushwa.
Amefafanua kuwa yeye alisimamishwa na maafisa wa Takukuru na kupekuliwa gari lake na kuchukua simu zake kwa ajili ya uchunguzi zaidi na siyo kukamatwa na maafisa hao Zungu ametaka magazeti hayo kuandika katika kurasa za kwanza habari za kukanushwa kwa kukamatwa kwake kinyume cha hapo atachukua mkondo wa sheria mahakamani.
Amedai kuwa habari hizo zimesumbua jamii ya Tanzania, ndugu zake na wapiga kura wake wa jimbo la Ilala jijini Dar es Salaam ukizingatia kuwa yeye ni kiongozi wa umma. Amesema kuwa habari hizi zimetumika kisiasa sana kwa nia ya kumchafua yeye asipite ujumbe wa NEC ya CCM kupitia jumuia ya wazazi.
CHANZO: Dewji Blog
0 comments:
Post a Comment