SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, November 6, 2011

HASSAN Shariff Atwaa Ubingwa Wa Mashindano Ya Mbio Za Baiskeli ya (Vodacom Tanzania Tanga Cycle Challenge 2011)

 Mshindi wa  kwanza  wa Kilomita 140 wa mbio za  baiskeli za “Vodacom Tanga cycle Challenge “  Hassan Sharif akimaliza mbio hizo kwa kwa kutumia masaa 4.13.07 .ambapo mbio hizo zilianzia katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga  hadi Hale na kurudi katika uwanja huo  hapo jana. 
Washindi wa kwanza na wapili wa mbio za Vodacom Tanga Cycle Challenge kwa upande wa kilometa 80 wakimaliza mbio hizo,ambapo Kudushi Nkandi  kushoto aliibuka mshindi na Mohamed Bundala akawa mshindi wa pili.
Baadhi ya washiriki wa mbio za baiskel za Vodacom Tanga Cycle Challenge wa kilometa 140 wakichuana vikali hapo jana.
 Baadhi ya washiriki wa mbio za baiskel za Vodacom Tanga Cycle Challenge wa kilometa 140 wakichuana vikali hapo jana mjini Tanga ambapo Hassan Sharif aliibuka mshindi kwa kutumia masaa 4:13.07 na kuzawadiwa fedha taslimu shilingi laki moja na nusu.
Washiriki mbio za Vodacom Tanga Cycle Challenge kwa upande wa walemavu wakimaliza mbio hizo hapo jana mjini Tanga.
Naibu Meya wa Mkoa wa Tanga Seleboss Mustafa  akimkabidhi fedha taslimu kiasi cha shilingi laki moja Mshindi wa kwanza wa mbio za  Vodacom Tanga Cycle Challenge wa kilomita 80,Kadushi Nkandi (kulia) mara baada ya kuibuka kidedea katika mbio hizo wapili toka kushoto Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude na msimamizi wa mawakala kanda ya Kaskazini Michael Kasun.
Naibu Meya wa Mkoa wa Tanga Seleboss Mustafa  akimkabidhi fedha taslimu kiasi cha shilingi laki moja  na nusu Mshindi wa kwanza wa mbio za  Vodacom Tanga Cycle Challenge wa kilomita 140,Hassan Sharif (kulia) mara baada ya kuibuka kidedea katika mbio hizo kwa kutumia  muda wa masaa 4:13.07 wapili toka kushoto Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude na msimamizi wa mawakala kanda ya Kaskazini Michael Kasun.
Naibu Meya wa Mkoa wa Tanga ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya elimu ,afya na uchumi,  Seleboss Mustafa, (kushoto)akimkabidhi  shilingi 75,000.mshindi wa  tatu wa mbio za Vodacom Tanga cycle  Challenge kwa upande wa Kilomita 140 Revocatus Sebastian, aliyetumia  Masaa 4: 15.52 mashindano hayo yaliyoanzia katika uwanja wa Mkwakwani  mjini Tanga  hadi Hale na kurudi katika uwanja huo ,wanaoshuhudia wapili kutoka kushoto ni Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude,Michael Kasun ambae ni msimamizi wa mawakala wa Vodacom kanda ya Kaskazini.
Mwaandaaji wa Mbio za baiskel za Vodacom Tanga Cycle Challenge Sophy Wakati akijadiliana jambo na Meneja Uhusiano na Habari za Mtandao wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu  kushoto kabla ya mbio hizo kuanza,wa pili kutoka kushoto Buruhani Yakub ambae ni  Mwandishi wa Habari wa Mwananchi Communication na Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude.

0 comments:

Post a Comment