SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, March 7, 2011

Majeshi ya Gaddafi yazuia waasi

Waasi wa Libya.
Majeshi ya serikali ya Libya yanasogea kuelekea kwenye bandari ya mafuta ya Ras Lanuf, yakiwasukuma waasi upande wa magharibi.
Mji wa Bin Jawad, uliopo kilomita 50 kutoka Ras Lanuf, sasa unadhibitiwa na majeshi yanayomtii kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi.
Umoja wa Mataifa umemtaja aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Jordan kama mjumbe wake nchini Libya, ambapo waasi wanaompinga Gaddafi wakipambana katika wiki yao ya tatu.
Umoja huo pia ulisema, takriban watu 200,000 wamekimbia ghasia hizo.
Unatoa wito wa kutolewa dola za kimarekani milioni 162 ili kusaidia watu 600,000 wanaoishi ndani ya Libya watakaohitaji msaada wa kibinadamu, na pia watu 400,000 wanaoondoka nchini humo kwa muda.

0 comments:

Post a Comment