SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, August 25, 2010

Ban Ki-Moon akasirishwa na ubakaji wa wanawake uliofanywa na waasi wa Kihutu DRC

Sample Image
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameeleza kukasirishwa mno na ubakaji wa wanawake uliofanywa na waasi wa Kihutu huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuamua kutuma mjumbe maalumu kufuatilia kadhia hiyo. Kwa mujibu wa msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Martin Nesirky, kwa uchache raia 154 wa Congo walibakwa wakati wa shambulio lililofanywa na waasi wa Kihutu wa Rwanda. Hata hivyo kwa mujibu wa maafisa wengine wa Umoja wa Mataifa wanawake 179 wamenajisiwa katika kipindi cha majuma ya hivi karibuni. Nesirky amevielezea vitendo hivyo kuwa mfano mwingine wa ngono za utumiaji nguvu na ukosefu wa usalama unaotawala nchini Congo. Ameongeza kuwa kutokana na uzito wa suala hilo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameamua kumtuma huko nchini Congo Atul Khare ambaye ni Naibu wake anayeshughulikia Operesheni za Kusimamia Amani.

0 comments:

Post a Comment