SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, June 6, 2010

ZAIN FASHION FOR EDUCATION BENEFIT LAFANA!!!


Miss Universe Tanzania 2010 Hellen Dausen katika pozi jukwaani kwa ajili ya kupata picha akiwa na vazi la Mmbunifu wa Mavazi kutoka nchini Afrika Kusini, David Tlale ambapo vazi hilo liliuzwa kwa tsh.milioni moja katika kuchania shule ya Kisarawe.
Model akipita jukwaani na Vazi la ubunifu kutoka kwa mbunifu David Tlale wa nchini South Africa aliyekuja kumpa company mbunifu mwenzake Ally Rehmtullah katika Fundraising ya Zain Fashion show for Education iliyofanyika jana katika hotel ya Double Tree,Masaki.
Model akiweka pozi kwa ajili ya picha katika Zain Fashion for Education Kampeni iliyokuwa ikiendeshwa kwa ajili ya kuchangia Shule ya Kisarawe ambapo jana ilifikia tamati .
Mwananimitindo David Tlale kutoka Nchini South Africa aliyekuja kumpa company swahiba wake Ally Rehmtullah akipita jukwaani na Model wake Jamilah ambaye amevaa vazi la ubunifu wake.
Vijana wanaokuja kwa kasi ya juu kutoka THT wakitoa buradani katika Zain Fashion for Education iliyorfanyika jana jijini Dar es Salaam.
Moja ya mavazi aliyoonyesha mwanamitindo Taibo Bacar kutoka Msumbiji.
Miss Universe Tanzania 2010 Hellen Dausen akkiwaonyesha wageni mbalimbali waliohudhuria Fashion for Education ni vazi la Mmbunifu wa Mavazi kutoka nchini Afrika Kusini, David Tlale ambapo vazi hilo liliuzwa kwa Tsh.milioni moja ambapo hotel ya Double Tree Hotel ilinunua vazi hiyo kwa ajili ya kuchangia Shule ya Kisarawe
Moja ya mavazi alilobuni mwanamitindo Ally Rehmtullah
Modo akipita jukwaani kwa mwendo wa Ngamia na Vazi lililotengenezwa na Mwanamitindo Ally Rehmtullah.
Mwamitindo Ally Rehmtullah akipita jukwaani ameambatana na Model aliyevaa ubunifu wake kuwashukuru wageni waliohudhuria Onyesho hilo.
Models walivaa mavazi aliyobuni Ally Rehtullah wakipita jukwaani kuaga ma kuwashukuru wageni waliohudhuria Zain Fashion for Education kwa ajili ya kuchangia shule ya Kisarawe ambayo ina uhaba wa madarasa na walimu na maizngira yake hayaridhishi kwa watoto kusoma fedha zilizopatikana katika kampeni hiyo zitasaidia kuboresha mazingira ya shule hiyo na kuongeza walimu wa kutosha hii yote ni kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu tuwe na vijana wasomi nchini kwetu Big up Ally Rehmtullah.
Kutoka kushoto ni Bang Magazine Manager Mrs.Emelda Mwamanga Mtunga akifuatiwa na Mr & Mrs Rakim wadau walipendeza sana.
Dada Mwavita Makamba Mkurugenzi wa Vodacom Foundation(mwenye miwani)akitiao story na rafiki yake katika Onyesho la Fashion for Education katika Hotel ya Double Tree jijini Dar es Salaam.
Kutoka kushoto ni Jokate Mwengelo Miss Tanzania 2007 akiwa na Binamu yake,Mwanamuziki wa Kizazi kipya Shaa pamoja na Manager wake Mmiliki wa Studio za MJ Records Master Jay katika Zain Fashion Show for Education.
Kulia ni mmoja wa wabunifu wa mavazi mahiri hapa bongo,Mustafa Hassanal.Dada Mwamvita Makamba kutoka VODACOM pamoja na Mdau wa mavazi hapa bongo mbele ya Camera ya MO BLOG
Mr & Mrs Rakim pamoja na Wadau wa mambo ya urembo wakishow love mbele ya Camera ya MO BLOG
Zainul akishow love na Marketing Manager Zain Bw.Constantine Magavilla pamoja na Mdau mbele ya Camera ya MO BLOG.
MC Evans Bukuku ndiye aliyekuwa mshereshaji siku ya jana Katika pozi na Aunty Ezekiel.

Kutoka kushoto mrembo wa Tanzania na Afrika 2005, Nancy Sumari, mwanamitindo Taibo Bacar kutoka Zimbambwe, mwanamitindo kutoka Tanzania Ally Rehmtullah pamoja na mmoja ya wadau kutoka Mo blog.
mohamed blog

0 comments:

Post a Comment