SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, March 15, 2014

UFUNGUZI WA WARSHA YA WADAU KUJADILI TAARIFA YA TATHIMINI YA ATHARI ZA KIJAMII NA MAZINGIRA YA MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA NGERENGERE HADI KIDUNDA

 Baadhi ya wajumbe wa bodi ya Dawasa wakisikiliza 
hotuba ya mgeni rasmi 
 Baadhi ya wataalamu wa washauri miradi mitatu inayotakiwa kutekelezwa ya ujenzi wa Bwawa la Kidunda wakwemo wa kutoka nje ya nchi wakijandaa kuwasilisha ripoti ya utafiti wa miradi hiyo kwa wadau.
 Baadhi ya watendaji wa wizara ya maji pamoja na Mamlaka za Dawasa na Dawasco katika picha ya pamoja na viongozi wakuu wakwemo wakuu wa Mikoa ya Moro, Pwani na Dar es salaam
 Hakuna kulala katika kupata picha za kumbukumbu.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( kushoto) akisalimana na mwezake wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadiki.
You have one new message.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadiki akitoa maelezo machache kuhusu suala la upatikanaji wa maji Mkoani mwake.
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwatumu Mahiza , akitoa salamu pamoja na umuhimu wa ushirikishwaji wadau mbalimbali katika kulinda mazingira na vyanzo vya maji.
 Viongozi wa juu wa Dawasa wakiteta jambo
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Kibena Kingo ( kulia ) akimsikiliza mwezake kabla ya kuanza kwa warsha.
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwatumu Mahiza ( kushoto) akisalimana na mwezake wa Dar es Salaam, Mhe Saidi Mecky Sadiki na aliyekati kati ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Amanzi.
 Baadhi ya wadau wa Vijij vya Kidunda, wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa juu wa Serikali kutika Wizara ya Maji, Dawasa na wakuu wa mikoa ya Moro, Dsm na Pwani.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Dawasa kwenye
 picha ya pamoja na Viongozi wa serikali
 Baadhi ya wajumbe wa bodi ya Dawasa wakisikiliza 
hotuba ya mgeni rasmi. Picha na John Nditi
 =====*****=====
Na John Nditi, Morogoro 
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Joel Bendera amefungua warsha ya wadau kujadili taarifa ya tathimini ya athari za kijamii na mazingira ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Ngerengere hadi Kidunda kwa kiwango cha changarawe, ujenzi wa mtambo mdogo wa kufua umeme wa megawati 20 na njia ya umeme kutoka Kidunda hadi Chalinze.
 Dk Bendera amezindua warsha hiyo katika ukumbi wa hoteli ya Nashera ya Mjini Morogoro , kwa niaba ya Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe. 
 Warsha hiyo ya siku moja pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe Mwatumu Mahiza, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Saidi Mecky Sadiki, wabunge wa Mkoa wa Morogoro akiwemo wa Jimbo la Morogoro Kusini,I nnocent Kalongeries , na Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Mhe Said Amanzi na wawakilishi wa makundi mengine 14 likiwemo la viongozi wa wananchi wa vijiji na kata zinazopitiwa na miradi hiyo. 
 Kwa mujibu wa hotuba ya Waziri huyo iliyosomwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, kuwa wazo la kujenga bwawa la Kidunda kwa ajil ya matumzi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za maji ya Jiji la Dar es Salaam , lililokuwepo muda mrefu. 
 Hivyo alisema kukamilika na kuanza kutumika kwa barabara na mtambo mdogo wa umeme na hatimaye ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme huo kutoka Kidunda hadi kituo cha umeme chalinze , kutatoa fursa mbalimbali za kuchumi na kijamii katika maeneo ya mradi huo.