SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, March 15, 2014

RIDHIWANI KIKWETE AANZA KAMPENI KWA KISHINDO JIMBO LA CHALINZE

Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubi wananchi wa Kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo,wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza rasmi jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubi wananchi wa Kijiji cha Saadani,Wilayani Bagamoyo.wakati wa kampeni zake zilizoanza rasmi jana Machi 14,2014.
Baada ya kumaliza Mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Matipwili,Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete alifika katika Kijiji cha Gongo ndani ya Tarafa ya Saadani na kukutana na wananchi wa Kijiji hicho na kuzungumza nao kama aonekanavyo pichani.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wanakijiji wakazi wa Kijiji cha Mkange,Saadani Wilayani Bagamoyo waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza huku wengi wakiahidi kumpa kura zao pindi itakapofika siku ya Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo hilo.
Diwani wa Kata ya Talawanda ndani ya Jimbo la Chalinze,Said Zikatimu akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Gongo,huku akiwataka kutofanya ajizi pindi itakapofika siku ya Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,hivyo kura zao zote wampigie Mgombea wa CCM ambaye ni Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete.
Diwani wa Kata ya Mkange,Ndg. Abdallah Mwendali nae hakuwa nyuma katika kuwasisitiza wananchi wa Jimbo la Chalinze.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akinong'onezwa jambo na Mmoja wa kinamama wa Kijiji cha Matipwili (Jina lake halikuweza fahamika mara moja).
"Ni furaha tupu" Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akifurahia jambo na wanakijiji wa Matipwili.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akisalimiana na Wanakijiji cha Mkange,wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Mkutano.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akisalimiana na Sheikh wa Kijiji cha Mkange.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akisalimiana na rafiki yake wa kitambo.
Mwenyekiti wa Kampeni katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Saleh Mpwimbwi akimmwagia sifa kede kede Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete .

==========================================================================

RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA NA HARAKATI ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE

Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akitoa hotuba yake kwa wakazi wa Kijiji cha Miono,Wilayani Bagamoyo leo Machi 15,2014,ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa Mikutano ya Kampeni zake za Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo la Chalinze unaotarajiwa kufanyika Aprili 6,2014.Picha zote na Othman Michuzi.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete pamoja na Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Steven Kazidi wakiwa na Mama wa Mbunge wa Zamani wa Jimbo la Chalinze (aliefariki Dunia),Marehemu Said Bwanamdogo wakati walipofika kumjulia hali nyumbani kwake Kijijini Miono,Bagamoyo leo Machi 15,2014.

Meneja wa Kampeni katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Steven Kazidi akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa Kumpigia debe Mgombea Ubunge katika Jimbo hilo,Ridhiwani Jakaya Kikwete (hayupo pichani),uliofanyika leo Machi 15,2014 kwenye Kijiji cha Kimange.

"Kinamama huko,inamaana hakuna vigelegeleeeee .....???" hivyo ndivyo alivyokuwa akiuliza Diwani wa Kata ya Kimange,Hussein Hading'oka (pichani) wakati alipokuwa akimwaga sifa kede kede kwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete.

Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa Kijiji cha Kimange,Kata ya Kimange,Wilayani Bagamoyo leo Machi 15,2014, wakati akiwasili kwa ajili ya Mkutano wa Kampeni zake za Uchaguzi huo mdogo unaotarajiwa kufanyika Aprili 6,2014.Picha zote na Othman Michuzi.

Meneja wa Kampeni katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Steven Kazidi (kulia) akizungumza jambo na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete kabla ya kumpatia kipaza sauti ili aweze kuzungumza na wanakijiji wa Kimange.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Kimange,Kata ya Kimange Wilayani Bagamoyo leo Machi 15,2014,wakati wa Mkutano wa Kampeni zake za Uchaguzi huo mdogo wa Jimbo hilo unaotarajiwa kufanyika Aprili 6,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akijumuika pamoja na wanakijiji wa Miono,Wilayani Bagamoyo kwenye dua maalum ya kumuomba Mwenyezi Mungu ajaalie mafanikio mema katika kumuongoza Mgombea Ubunge huyo kwenye mwendelezo wa Kampeni zake.
Dua ikiendelea.......
wakiwa wamesimama kwa dakika moja kumkumbuka aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze,Marehemu Said Bwanamdogo.
"Shkamoo Bibi....."
Ridhiwani akiendelea kumwaga sera zake.

Wananchi wakifatilia Hotuba ya Mgombea wao kwa Umakini mkubwa.
Wadau wa Kijiji cha Kimange wakichukua taswira ya Mgombea wao kupitia simu zao za mikononi.
"Mtoto Mzuri naomba Kofiaaaaa"
Wananchi wakimsikiliza Mgombea wako kwa makini.
Nyundo na Jembe ndio mpango mzimaaaa......
"Kijana wetu wewe ndie tunaekutaka,na amini utashinda kwa kishindo" ndivyo alivyosikika mama huyu akimwambia Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete.
Mkutano kwa siku ya leo ulimalizikia katika Kijiji cha Mbwewe,Pichani ni Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze akipita katikati ya vijana wa chipukizi wakati akiwasili kwenye Kijiji hicho.
Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete (kulia) akifurahia baada ya kupewa maneno ya kuvutia kutoka kwa vijana wa chipukizi.