SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, March 11, 2014

Hali si shwari katika Makao Makuu ya Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Arusha baada ya kuibuliwa kwa tuhuma za wizi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya maofisa wawili wa ngazi za juu.

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Enos Bukuku (kulia) akimwongoza Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Natu Mwamba, jana jijini Arusha wakati wa uzinduzi wa mradi wa Mfumo wa Malipo kwa nchi za Afrika Mashariki. Picha na Filbert Rweyemamu.  
----
 Hali si shwari katika Makao Makuu ya Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Arusha baada ya kuibuliwa kwa tuhuma za wizi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya maofisa wawili wa ngazi za juu.

Maofisa hao ni Naibu Katibu Mkuu (Fedha na Utawala), Jean-Claude Nsengiyiyumva anayetuhumiwa kujichotea malipo ya posho ya vikao kwa kujiandika kwenye orodha ya washiriki wa vikao vitatu tofauti vinavyofanyika kwa wakati mmoja bila kuhudhuria na Ofisa Milki Mwandamizi, Phil Klerruu anayetuhumiwa kuchukua mali za jumuiya kinyume cha sheria.

Wakizungumzia tuhuma dhidi yao kwa nyakati tofauti, Nsengiyumva na Klerruu walikana huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake kuratibu mikakati ya kumchafua mwenzake.
“Sina hofu na tuhuma zinazoelekezwa dhidi yangu kwa sababu hazina ukweli. Nimesikia SG (Katibu Mkuu), ameunda kamati kunichunguza ingawa sina taarifa rasmi. Ngoja tusubiri kwa sababu ukweli wote utadhihirika,” alisema Nsengiyumva.
Naibu Katibu Mkuu huyo anadaiwa kumtumia Katibu Muhtasi wake, Caroline Mudambo kumsainia katika orodha ya washiriki wa vikao ambavyo hakuhudhuria.
Nsengiyumva ambaye amekuwa katika wadhifa huo kwa miaka mitano tangu alipoteuliwa na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi mwaka 2009, pia anatuhumiwa kugoma kuidhinisha mikataba mipya ya baadhi ya wafanyakazi kutokana na chuki na masuala binafsi.Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.....

0 comments:

Post a Comment