SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, June 3, 2013

AJALI MBAYA YATOKEA MKOANI MBEYA, WATU WANNE WAHOFIWA KUFA

 GARI LA ABIRIA AINA YA HIACE IKIWA IMEGONGANA USO KWA USO NA GARI AINA YA LAND CRUISER 
 
HIZI NI BAADHI YA MAITI ZILIZO OKOLEWA PUNDE BAADA YA AJALI KUTOKEA 

 
HIVI NDIVYO DALADALA HII ILIVYO HARIBIKA BAADA YA AJALI HIYO KUTOKEA 
 
DALADALA IKIWA IMEUMIA VIBAYA 
 
HILI NDILO ENEO AMBAPO AJALI HIYO IMETOKEA 
WANANCHI MBALIMBALI WAKIWA KATIKA ENEO LA TUKIO KUSHUHUDIA AJALI HIYO
 TINGO WA DALADALA AKIWAANASHUSHWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA 

 TINGO WA DALADA\LA AKIWA ANAPELEKWA KATIKA MSAADA WA HARAKA RUFAA 
 MMOJA WA ABIRIA AKIKIMBIZWA KATIKA MSAADA WA HARAKA RUFAA 
MWILI WA DEREVA WA DALADALA ALIYE FARIKI PAPO HAPO UKIPELEKWA CHUMBA CHA KUHIFADHIA MAITI RUFAA
Kaimu kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ndugu Barakaeli Masaki akizungumza na waandishi wa habari.
Picha na Habari na JOSEPH MWAISANGO

Watu sita wamefariki Dunia na wengine Sita kujeruhiwa katika ajali ya Barabarani iliyo tokea Nanenane Darajani eneo la Uyole Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mbeya Barakael Masaki amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuwataja marehemu hao kuwa ni pamoja na madereva mmoja wa Hiace. 

Masaki amesema dereva wa Hiace amefahamika kwa jina la Meshack Hosea aliye kuwa anaendesha Gari nambali T178 AAV aina ya Toyota Hiace inayofanya kazi Sokomatola na Uyole ambapo muda huo ilikuwa ikitokea Sokomatola kuelekea uyole.

Dereva wa Toyota Land Cruiser Abdalah Ndabagi anashikiliwa na Polisi kwa Mahojiano.

Maiti nne hazijatambuliwa hadi sasa wakiwemo wanawake wanne waliokuwa abiria katika Daladala hiyo na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa jijini Mbeya.

Aidha amesema majeruhi sita wamelazwa katika hospitali ya Rufaa wakiwemo wanaume watano na Mwanamke mmoja . Ambao mpaka sasa majina yao hayatambuliwa kutokana na kujeruhiwaa vibaya.

Chanzo cha ajali hiyo kimetajwa kuwa ni  mwendo kasi wa Magari hayo na wito ameutoa kwa Madereva kuwa makini na kufuata sheria za Barabarani ili kuepusha ajali ambazo zingeweza kutokea. Ikizingatiwa hilo ni eneo la Jiji.

Picha na Mbeya yetu Blog
)

0 comments:

Post a Comment