Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na baadhi ya marais wakuu wa nchi
za Umoja wa Afrika AU wakimpongeza Rais mstaafu wa Brazil Lula Da Silva
kwa hotuba yake aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 17 wa Wakuu
wa nchi za AU uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Sipopo,jijini
Malabo,Equatorial Guinea leo asubuhi.Hotuba hiyo ya kusisimua ilitilia
mkazo kwa nchi za Afrika kushirikiana ili kujiletea maendeleo na kuepuka
misaada yenye masharti inayolididimiza bara la Afrika katika lindi la
umaskini.
Rais
Jakaya Kikwete akishiriki kupanda mti wakati wa ufunguzi rasmi wa
mkutano wa Wakuu wa Umoja wa Afrika(AU) katika mji mkuu wa Guinea ya
Ikweta, Malabo.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akishiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa 17
wa Umoja wa Afrika unaofanyika jijini Malabo, Equatorial Guinea.
(Picha na
Freddy Maro-IKULU)
0 comments:
Post a Comment