SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, September 25, 2010

Watu wengi duniani wanakubaliana na hoja za Rais Ahmadinejad kuhusu tukio la Sept 11

Sample Image
Siku ya Alhamisi Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliuambia ulimwengu kuwa tukio la Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani bado lina utata na hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa lilikuwa shambulizi la kigaidi. Tamko hilo la Rais wa Iran lililowakasirisha mno watawala wa Washington limepata uungaji mkono kutoka kila pembe ya dunia. Katika miaka ya huko nyuma tafiti mbali mbali zilionyesha kuwa watu wengi wanaamini kuwa Marekani na Utawala haramu wa Israel kwa pamoja zilishirikiana katika kupanga tukio hilo. Nchini Jordan asilimia 31 ya wananchi wanaamini kuwa tukio hilo lilifanyika ima kwa msaada wa Marekani au kwa ridhaa yake na nchini Misri asilimia 46 pia wanaamini hivyo. Mrekani kwenyewe uchunguzi wa maoni wa mwaka 2006 uliofanywa na shirika la Scrippsnews ulifichua kuwa asilimia 36 ya Wamarekani wanaamini kuwa serikali yao ilihusika kwa njia moja au nyingine katika utekelezaji wa tukio hilo. Rais Mahmoud Ahmadinejad ametoa changamoto kwa Umoja wa Mataifa kuanzisha uchunguzi huru kuhusu tukio hilo.

0 comments:

Post a Comment