Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametoa wito wa kuongezewa mataifa mawili ya barani Afrika katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa UNSC. Akizungumza katika kongamano kuu la Umoja wa Mataifa hapo jana mjini New York Marekani, Rais Mugabe amesema, mataifa hayo yanafaa kujumuishwa kama wanachama wa kudumu wa baraza hilo na kupewa haki ya veto ili kuwa sauti itakayoyawezesha kupaza changamoto zinazozikabili nchi za bara hilo. Mugabe amekosoa sera na kanuni zinazoendesha baraza hilo na kutaka zifanyiwe marekebisho au zibadilishwe. Aidha, ameyataka mataifa yanayotajwa kuwa yenye uwezo mkubwa duniani yakomeshe unafiki wao wa kuhubiri demokrasia huku yakifeli kutekeleza ahadi zao.
0 comments:
Post a Comment