SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, September 24, 2010

MKUTANO WA KUHAMASISHA WAISLAM KWENDA HIJJA

Na Mary Kweka - Maelezo.
Taasisi ya kiislam ya Tanzania Hajj Mission ikishirikiana na ubalozi wa Iran Inchini imeandaa mkutano wa kimataifa utakaofanyika Jijin Dar es salaa, wenye lengo la kutoa semina ya Hijja na umoja wa Umma wa Kimataifa wa Kiislam na kuwahamasiha waislamu kujua masuala mbalimbali yahusuyo Ibada ya Hijja.
Hayo yamesemwa jana jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa taasisi hiyo Shekhe Khalid Mohammed Mrisho wakati akizungumza na wandishi wa habari juu mkutano huo utafanyika tarehe 26 hadi 27 mwezi huu jijini Dares salaam.
Alisema kuwa mkutano huo unalenga kuhamasisha Idadi ya Watanzania wengi kushiriki Ibada ya Hijja ili kutimiza idadi rasmi iliyotolewa na Serikali ya Saudi Arabia.
“Watanzania wanaoenda Hijja kila mwaka hawazidi 2000 wakati nafasi tunayokuwa tumeandaliwa na serikali ya Saudi Arabia ni watu 30,000, hivyo tumeona upo umuhimu wa kuwahamasha waislamu wa Wa tanzania kijitokeza kwa wingi japo kufikia 2500 mwaka huu”.
Akizitaja mada zitakazoongelewa kwenye majadala huo , Shekhe Khalid Mohammed amesema ni Kumkumbuka Allah(swt)katika Hijja na Faida nyingine za Hijja, Falsafa ya Hijja, Hijja na kisimamo cha watu,Hijja na haki za binadam duniani na Hadhi ya mwanamke na Sayyida Hajar katika Hijja.
Zingine alizozitaja ni Uwezo wa utekelezaji waa Ibada ya Hijja katika Afrika, Taratibu za Hijja na wananyokubaliana baina ya Sunni na Shia,Hijja na Siasa, Fursa na vikwazo vya Hijja katiak Afrika na kuunda Utamaduni wa hamu ay Hijja miongoni mwa waislam wa Afrika .
Aidha Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa Mkutano huo pia utahamasisha kujenga umoja wa kimataifa wa Umma wa Kiislam kwa Tanzania na nchi zingine za kiislam duniani.
Kwa upande wa Balozi wa Iran inchin Bwana Mohsen Movahhed Ghomi amesema Serikali ya Irani inashirikiana na Tasisi ya Tanzania Hajj Mission kuhakikisha Waislamu wa Tanzania wanapata uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa kwenda Hijja na kujitokeza kwa wingi kufanya Ibada hiyo kila mwak
Ibada hii ya hijja, ni moja kati ya nguzo tano za Uislam na kwamba wanaopaswa kuitekeleza ni wale wenye uwezo na kwa wale wasiokuwa nao hawalazimishwi kuhiji, ni Ibda inayofanyika kwa waislamu kutembelea sehemu tukufu za Saudia Arabia na Mecca na hufanyika kila mwaka .

0 comments:

Post a Comment