SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, September 24, 2010

Mahakama ya Kenya yawapata na hatia ya uharamia Wasomali 7

Sample Image
Mahakama ya Mombasa nchini Kenya imewapata na hatia ya kufanya uharamia Wasomalia 7 na kuwahukumu kifungo cha miaka mitano jela kwa kuteka nyara meli ya Uhispania mwaka 2009. Wasomalia hao wamehukumiwa baada ya kutiwa mbaroni mwezi Mei mwaka uliopita. Suala la kuwahukumu maharamia wa Kisomali wanaokamatwa limekuwa likikwamishwa na kuzusha hitilifau za mitazamo juu ya nchi gani wahukumiwe maharamaia hao. Somalia yenyewe haina vyombo vya sheria vya kuendesha kesi hizo. Kenya ina wasiwasi kuwa maharamia wanaoachiliwa baada ya kutumikia vifungo vyao jela na wale wasiopatikana na hatia watalundikana nchini humo, na suala hilo kuhatarisha usalama wa nchi hiyo. Kuna maharamia wa Kisomali 15 wanaotumikia kifungo nchini Kenya huku mamia ya wengine bado wakiwa wanaendelea kushikiliwa. 

0 comments:

Post a Comment