SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, September 30, 2010

GENEVIEVE AKABITHIWA BENDERA YA TAIFA
Genevive Emmanuel akiwa ameshikilia bendera ya taifa mara baada ya kukabidhiwaa rasmi tayari kwa safari yake ya kuelekea nchini China leo. Vodacom Miss Tanzania, Genevieve Emmanuel Mpangala,jana alikabithiwa Bendera ya Taifa tayari kwa safari yake ya kuelekea nchini China katika jiji la Sanya ambako shindano la dunia Miss World 2010 linatarajiwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu. Genevieve ataondoka leo kwa ndege ya Shirika la Quatar Airways akipitia Uarabuni, Mongolia na kisha Sanya nchini China. 
Mwenyekiti wa Sekta Binafsi na aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi bendera ya taifa kwa Vodacom Miss Tanzania 2010, Esther Mkwizu (wa pili kushoto) akikabidhi bendera hiyo huku wazazi wa Genevive wakishuhudia, kulia ni baba yake Bw. Emmanuel Mpangala na kushoto ni mama yake Mary.

0 comments:

Post a Comment