SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, July 16, 2010

Waliofanya njama za kumpindua Rais Jammeh wahukumiwa adhabu ya kifo
Sample Image Jaji wa Mahakama Kuu ya Gambia amewahukumu watu wanane akiwemo mkuu wa zamani wa majeshi ya nchi hiyo adhabu ya kifo baada ya kupatikana na hatia ya kupanga njama mwaka jana za kumpindua Rais Yahya Jammeh wa nchi hiyo. Jaji Emmanuel Amadi amesema kuwa, watu hao wanaruhusiwa kukata rufaa katika kipindi cha siku 30 zijazo. Hii si mara ya kwanza kwa maafisa wa jeshi la Gambia kupanga njama za kumpindua Rais Jammeh. Rais Yahya Jammeh aliingia madarakani mwaka 1994 akiwa afisa kijana wa jeshi la nchi hiyo na alikuwa na cheo cha Luteni, na ameendelea kuiongoza nchi hiyo ndogo iliyoko Magharibi mwa Afrika, baada ya kushinda vipindi vitatu vya uchaguzi wa rais. Taarifa zinasema kuwa, Langtombong Tamba mkuu wa zamani wa majeshi, Lamin Bo Badjie mkuu wa zamani wa upelelezi na Modou Gaye msaidizi wa mkuu wa zamani wa jeshi la polisi nchini humo ni miongoni mwa maafisa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu ya kifo. 
**************************** 

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kutembelea Uganda na Sudan
Sample ImageScott Gration Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa ameanza safari ya mzunguko itakayomchukua muda wa wiki mbili kwa kuzitembelea nchi za Sudan na Uganda kwa shabaha ya kuchunguza kwa karibu migogoro na machafuko yaliyotokea hivi karibuni katika nchi hizo. Katika safari yake hiyo, Gration anatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo na maafisa wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika nchini humo na hali kadhalika kushauriana na wajumbe kutoka Russia, China Uingereza, Ufaransa na Norway walioko nchini Sudan kuhusiana na migogoro ya Darfur na kusini mwa Sudan. Hali kadhalika atakutana na viongozi wa chama tawala cha National Congress na kile cha Sudan People's Liberation Movement SPLM kuhusiana na uitishwaji wa kura ya maoni iliyopangwa kufanyika mapema mwakani. Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa ataitembelea Uganda na kujadili na viongozi wa Kampala mikakati ya kuisaidia nchi hiyo katika kukabiliana na mashambulizi ya makundi ya kigaidi, na mpango wa kutumwa askari zaidi kikosi cha kulinda amani nchini Somalia.
http://kiswahili.irib.ir/

0 comments:

Post a Comment