SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, July 25, 2010

Maadhimisho Ya Siku Ya Mashujaa Leo
Rais Jakaya Kikwete pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis Mwamunyange na viongozi wengine wa jeshi wakitoa heshima zao leo wakati wa maadhimisho ya siku ya kuwakumbuka mashujaa waliopigana vita kuu ya Dunia 1939-1943.maadhimisho hayo yamefanyika leo asubuhi katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis Mwamunyange akielekea kutoa heshima za kijeshi kwa kuwakumbuka mashujaa waliopigana vita kuu ya Dunia 1939-1943,Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam leo.Rais Kikwete akiongoza viongozi mbalimbali katika maadhimisho ya kuwakumbuka mashujaa waliopigana vita kuu ya dunia 1939-1943,Mnazi mmoja leo.Askari wa JWTZ wakitoa heshima za kijeshiRais Jakaya Kikwete akiweka ngao na mkuki kwenye mnara uliopo Mnazi mmoja wakati wa maadhmisho ya siku ya mashujaa,yaliyofanyika leo.kiongozi wa mabalozi akiweka shada la maua.Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wazee waliopigana vita kuu ya dunia 1939-1943 katika viwanja vya Mnazi mmoja leo.Rais Aman Karume akisalimiana na wazee.Rais Mstaafu wa awamu ya pili,Alhaj Ally Hassan Mwinyi akifuatiwa na Waziri Mkuu mstaafu,Mh. Fredrick Sumaye na viongozi wengine walipokuwa wakiwasalimia wazee waliopigana vita kuu ya Dunia 1939-1943 katika maadhimisho ya siku ya mashujaa leo.Gwaride kwa Askari wa JWTZGwaride kwa Askari wa FFU

0 comments:

Post a Comment