SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, May 8, 2010

Vigogo BoT wafutiwa mashitaka

Na Amina Magona, Ilala
UPANDE wa mashitaka katika kesi inayowakabili wakurugenzi wanne wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), leo umeafutia mashitaka yaliyokuwa yakiwakabili vigogo hao na kuwafungulia mengine mapya.
Kesi hiyo ilikuwa inasikilizwa leo asubuhi mbele ya Hakimu Mkazi, Agnes Mchome.
Wakurugenzi hao—Simon Jengo ambaye ni Mkurugenzi wa BoT; Naibu Mkurugenzi wa Fedha za Nje, Kisima Mkango; Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kitengo cha Sheria; Bosco Kimela na Mkurugenzi wa Huduma za Benki, Ally Bakari—wanatuhumiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi.
Wakili wa Serikali, Afrey Sedekia, amedai kuwa washitakiwa hao kati ya mwaka 2004, 2005 na 2007 walitumia madaraka yao vibaya kwa kuchapisha noti nyingi bila idhini ya Serikali.
Awali washitakiwa hao ambao mashitaka yao yamefutwa walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Samwel Maweda na Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincon, wakikabilia na makosa ya kuhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya sh. bilioni 104.
Wakili huyo aliendelea kudai kuwa washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka matatu ambapo shitaka la kwanza linawahusu Jengo na Mlayo ambao ni washitakiwa wa kwanza na wa pili.
Katika mashitaka hayo inadaiwa kuwa washitakiwa hao walitumia nyaraka za Serikali kwa lengo la kudanganya miongozo kinyume cha kifungu cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa.
Imedaiwa kuwa washitakiwa hao wawili kwa pamoja mwaka 2004, wakiwa ni waajiriwa wa Serikali katika BoT ambako walikuwa wakishikilia nyadhifa zao za sasa waliongeza gharama za usambazaji wa noti ikilinganishwa na gharama halisi ya mwaka 2001 huku wakijua ni kosa kisheria.
Shitaka la pili linafanana na la kwanza ambapo linamhusu mshitakiwa wa kwanza, Jengo, anayedaiwa kutumia nyaraka hizo kumdanganya mwajiri wake ili aweze kuongeza gharama za uchapishaji wa noti mwaka 2005.
Katika shitaka la tatu imedaiwa kuwa kati ya mwaka 2004 na 2007 washitakiwa wote wanne kwa pamoja waliisababishia Serikali hasara ya sh. 104,158,536,146.
Washitakiwa hao wanadaiwa kuwa walitenda kosa hilo wakiwa waajiriwa wa ofisi ya umma baada ya kushindwa kutimiza wajibu wao kwa kutobaini maandalizi ya kuandaa mkataba ulioingiwa na BOT, wa kutengeneza noti mpya uliokuwa na gharama kubwa ikilinganishwa na hali halisi.
Hata hivyo kesi hiyo imefutwa na kubadilishiwa nyingine leo asubuhi.Kesi hiyo itatajwa tena Mei 21, mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment