SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, April 7, 2016

DKT. SHEIN AWAONGOZA VIONGOZI MBALIMBALI KATIKA DUA YA KUMUOMBEA MAREHEMU MZEE KARUME


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akijumuika na Viongozi na wananchi katika Hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Baadhi ya Wananchi wa Mjini na Mashamba waliojumika kwa pamoja katika Hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Baadhi ya Viongozi na Wananchi kwa pamoja wakiwa katika Hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Miongoni mwa Akinamama wakimuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume wakati wa Hitma iliyosomwa leo katika Osifi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na Wananchi mbali mbali wa dini tofauti.
Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwana Mwema Shein (katikati) Mama Fatma Karume (wa pili kulia) pamoja na Wake wa Viongozi wakiwa katika Hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Wanafunzi wa Madrasa kutoka Vyuo mbali mbali na wananchi waliohudhuria katika Hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe,Amani Abeid Karume,(wa pili kushoto) Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,Ali Hassan Mwinyi(wa pili kulia) Makamo wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania Mhe.Mohammed Gharib Bilali(kulia)kwa pamoja wakiitikia dua iliyoombwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheik Khamis Haji Khamis baada ya kumalizika kisomo cha Hitma ya dua ya kumuombea Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Sheikh Hamid Masoud Jongo kutoka Jijini Dar es Salaam akitoa mawaidha baada ya Hitma ya dua ya kumuombea Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akiweka shada la mauwa katika kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume baada ya kumalizika kisomo cha Hitma na dua ya kumuombea, iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,John Pombe Magufuli,kuweka Shada la mauwa katika kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume baada ya kumalizika kisomo cha Hitma na dua ya kumuombea, iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
KWA HABARI ZAIDI

0 comments:

Post a Comment