SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, October 9, 2014

AIRTEL YAZINDUA DILI KWA WASANII WOTE

Wasanii wa kundi la yamoto band wakiwa na msanii maarufu nchini ambae pia ni balazo wa airtel trace music stars tanzania Ommy Dimpos wakionyesha namba maalum itakayotumika kupiga na kutuma nyimbo kwa wasanii chipukizi kwenye shindano la airtel trace music stars lililozinduliwa rasmi jana.

Balozi wa airtel music stars Tanzania Ommy Dimpos akitangaza rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya airtel trace music star kwa kukerekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi jana Coco beach.
Meneja uhusiano wa airtel Jackson Mmbando akizindua na kutangaza rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya airtel trace music star kwa kukerekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi jana coco beach.
Baadhi ya wasanii waliojitokeza wakijaribu kuimba na kurekodi kwenye namba maalum ya kushiriki mashindano ya airtel trace music stars katika viwanja vya coco beach ambapo airtel ilimezindua rasmi namba ya kushirmaki shindano la airtel trace music stars kwa lengo la kuwasaidia wasanii wanaochipukia nao kufikia malengo yao ya kuwa nyota wa musiki.
Mmoja kati ya wasanii waliojitokeza akijaribu kuimba kwenye namba maalum ya kushiriki mashindano ya Airtel Trace Music Stars katika viwanja vya coco beach huku meneja uhusiano wa airtel Jackson Mmbando akishuhudia. Airtel imezindua mashindano haya ya Airtel Trace Music stars kwa lengo la kuwasaidia wasanii wanaochipukia nao kufikia malengo yao.

Wasanii wa kundi maarufu na linalofanya vizuri toka TMK yamoto band wakionyesha vitu vyao wakati wa hafla maalum ya uzinduzi wa namba maalum itakayotumika kupiga na kurekodi nyimbo na wasanii chipukizi ili kujishidia dili la kurediwa nyimbo zao marekani kupitia shindano maalum la airtel trace music stars katika viwanja vya coco beach jijini dar es salaam.
 
KAMPUNI ya simu za mkononi ya airtel imezindua rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya Airtel Trace Music Stars kwa kurekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi huku baadhi ya wasanii chipukizi wakipata nafasi yakuonyesha vipaji vyao katika viwanja vya Coco Beach

Akizungumza katika uzinduzi huo uliopambwa na burudani mbalimbali ikiwemo Yamoto bendi katika viwanja vya Coco beach jijini Dar es salaam meneja uhusiano wa airtel bw. jackson mmbando amesema kila mtanzania anayo nafasi ya kushiriki katika shindano hilo kwa kupiga simu namba 0901002233.

Aidha Mmbando ameongeza kuwa lengo la kuanzisha shindano hilo ni kuinua vipaji vya watanzania wenye kujua kuimba ili wapate nafasi ya kuwa staa wa kimataifa.

Nae balozi wa shindano hilo Ommy Dimpoz amewaomba watanzania kujitokeze kwa wingi katika kushiriki mashindano hayo ambapo mshindi atajinyakulia zawadi kabambe ikiwemo kurekodi na kusambaziwa nyimbo zake chini ya studio kubwa ulimwenguni pamoja na safari ya kwenda nchini marekani kwa ajili ya kupata mafunzo ya kimuziki na nguli wa muziki wa amerika Akon.
 

0 comments:

Post a Comment