SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, September 15, 2014

WAKAZI WA TABORA WALIPOKEA VYEMA TAMASHA LA FIESTA 2014

Msanii wa muziki wa kizaz kipya ambaye kwa sasa yuko chini ya kampuni ya No Fake Zone,Linah Sanga akiwa jukwaani sambamba na sahabiki wake wakicheza kwa pamoja ndani ya tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye kwa sasa yuko chini ya kampuni ya No Fake Zone,Linah Sanga akiwa jukwaani sambamba na madansa wake wakilishambulia jukwaa la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
Msanii mwingine anaekuja vyema kwenye anga ya muziki wa Bongofleva aitwaye Kadja ambaye anatamba na wimbo wake wa Maumivu niache akiimba pamoja na Linah
Wasanii chipukizi kutoka Tabora nao walionesha umahiri wao jukwaani
Sehemu ya umati mkubwa wa watu waliofika kulishuhudia tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
 Shilole nae akiimba sambamba na aliedai kuwa ndiye mchumba wake kwa sasa,Nuhu Mziwanda katika tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
 Maelefu ya wakazi wa mji wa Tabora waliojotokeza kulishuhudia tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
 Ilikuwa buruuudani ya kusambaza upendo wa kweli kwa wakazi wa Tabora ndani ya tamasha la Fiesta
 Shigiiiiidi shhheeeedddaaah...! Mtangazaji wa Clouds Fm,Adam Mchomvu akiwaimbisha wakazi wa mji wa Tabora na vitongoji vyake usiku wa kumkia leo katika tamasha la Fiesta lililofanyika ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
 Msanii anaefanya vyema katika anga ya muziki wa Bongofleva,Ommy Dimpoz akiwaimbisha mashabiki wake wimbo wa Nani kama mama.
 Kutoka THT,anaitwa Rachael akiimba jukwaani huku densa wake akinogesha mashabiki kimtindo.
Wasanii wa muziki wa hip hop ambao wanafanya vyema kwa sasa,Young Killer na Stamina kwa pamoja wakionesha umahiri wao wa kufoka foka mbele ya maelfu ya mashabiki wao (hawapo pichani),katika tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
Maelfu ya wakazi wa mji wa Tabora waliojotokeza kulishuhudia tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
Mkali wa mangoma kutoka Clouds FM,Dj Zero akikamua mangoma vilivyo.
Maelfu ya wakazi wa mji wa Tabora wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora
Msanii chipukizi wa kizaz kipya aitwaye BK kutoka Bukoba akiburudisha mashabiki wake (hawapo pichani) usiku wa kumakia lewo katika tamasha la Fiesta.
Mmoja wa wasanii aliyekuja kwa staili ya aina yake jukwaani,ajiitaye Director Shaibu akionesha vimbwanga vyake kwenye jukwaa la Fiesta huku miluzi na shangwe zikiwa zimetawala kila kona ya uwanja.
Msanii wa Bongofleva,Kadja akiimba wimbo wake wa Maumivu niache mbele ya maelfu ya wakazi wa Tabora (hawapo pichani) waliofika kwenye tamasha la Fiesta usiku wa kuamkia leo.
Anajiita Mo Music anaetamba na wimbo ake uitwao Basi Nenda akiwaimbisha mashabiki wake
Maelfu ya mashabiki wakishangweka vilivyo.
Mkali wa Bongo Hip Hop Farid Kubanda a.k.a Fid Q akikamua vilivyo juu ya jukwaa na la Fiesta
Palikuwa hapatoshi usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora,ambapo tamasha la Fiesta lilirindima.
Niki wa Pili kutoka kundi la Weusi akiwaimbisha mashabiki wake.

0 comments:

Post a Comment