Miss
Tanzania 2012, Brigitte Alfred akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango
wa kutoa elimu kwa wajasiliamali kwa albino 50, kushoto ni Kaimu katibu
Mkuu wa Jumuiya wa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), Mohamed
Chanzi.
Viongozi
wa Taasisi ya Brigitte Alfred Foundation, TAS na JAT katika picha ya
pamoja mara baada ya kuzinduzi mpango wa kusomesha albino 50 masomo ya
Ujasiriamali.
*********
Na Mwandishi wetu, Dar
Taasisi
ya ya Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred ijulikanayo kwa jina na
Brigitte Alfred Foundation (BAF) ikishirikiana na taasisi ya Junior
Achievement Tanzania (JAT) inazindua rasmi mafunzo ya ujasiriamali kwa
jamii ya Albino.
Akizungumza
katika uzinduzi huo jana, Brigitte alisema kuwa taasisi yake kwa
kushirikiana na JAT itaanza na mafunzo kwa albino 50.
Brigitte
alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga sehemu kuu mbalimbali ambazo ni
kujitambua (Life skills), kutathmini aina mbalimbali za biashara
(Business Analysis), namna ya kutunza pesa ( How to save), kuandika
mchanganuo wa biashara (Business Plan), kutembelea sehemu mbalimbali
zinazoendana na biashara atakayoifanya na jinsi ya kuanza biashara.
Alisema
kuwa BAF ikishirikiana na wadau mbalimbali na pia itagharimia gharama
za mafunzo na mahitaji mbalimbali ya kuboresha hali yao.
“Mafunzo
haya yatachukua muda wa mwaka mmoja yaani watashiriki na yataanza rasmi
Agosti 18, kila mshiriki wa mafunzo haya atapatiwa kitabu chenye masomo
yote
ili aweze kuendelea kujisomea,” alisema Brigitte.
Mkurugenzi
wa JAT, Maria Ngowi alisema kuwa wamejipanga kufanikisha mpango huo na
wanaamini albino watakaopata mafunzo hayo watafanikiwa katika maisha yao
ya kila siku.
Ngowi
alisema kuwa JAT imejikita katika Nyanja tatu ambazo ni ujasiria mali,
elimu ya kuzalisha, kuiwekeza na kutunza fedha na elimu ya kazi.
Alisema
kuwa taasisi yao ni sehemu ya taasisi kubwa ulimwenguni inayoitwa
Junior Achievement International ambayo iko katika nchi 120 duniani huku
afrika ikiwa katika nchi 17.
Kaimu
Katibu Mkuu wa Tanzania Albino Society (TAS), Mohamed Chanzi
alimshukuru Brigitte na JAT kwa kuwajali na kuomba wadau mbali mbali
kuwaunga mkono.
“Wamelenga
kutusaidia kimaisha, kwani msaada wa elimu ni mkubwa kulinganisha
misaada mingine, naomba wadau wawaunge mkono,” alisema Chanzi.
0 comments:
Post a Comment