SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, June 8, 2014

MBUNGE JOSHUA NASSARI NA ANANDE NNKO WAMEREMETA KWENYE KANISA LA PENTEKOSTE KILINGA,MERU

Msafara wa gari chache majira ya saa 2:30 ulianza safari katika viwanja vya Usa-River ambako gari za maharusi zilikuwa zikipambwa mdogo mdogo zikapanda Kilima zikiwa na maharusi Joshua Nassari na Anande Nnko safari ilikuwa ni kanisa la Kipentekoste la Kilinga,Meru tayari kwa ajili ya Ndoa.
Hatimaye Bw Harusi Joshua Nassari anateremka katika usafiri wake aina ya Range Rover muda mfupi baada ya kufika katika viwanja vya kanisala la Kilinga maarufu kama kwa Mchungaji Babu.
Wageni mbalimbali walihudhuria ibada hiyo ya ndoa mmoja wapo ni huyu ,Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai(katikati)
Bibi Harusi Anande Nnko alikuwa ni mwenye furaha kila wakati ,"Full Tabasamu."
Wenyeji katika shughuli hiyo akiwemo mzee Samweli Nassari ,baba mzazi wa Jishu walikuwa wamevalia mavazi nadhifu aina ya suti wakingojea ugeni uliokuwa ukiwasili katika kanisa la Kilinga.
Hataimaye Bw Harusi Joshua Nassari akaingia kanisani yeye na wapambe wake na hapa anaye ngojewa ni Bibi Harusi Anande Nko.
Bi Harusi Anande Nko akashuka katika gari alilokuja nalo aina ya Land Cruser VX.
Bwaa Harusi Joshua Nassari akamvisha pete mkewe Anande Nnko.
Bibi Harusi Anande Nnko akamvisha pete mumewe Joshua Nassari
Kisha Maharusi wakapongezana.
Maharusi wa wakawekewa mikono na Maskofu wakiongozwa na Askofu mkuu wa kanisa la Pentekoste Tanzania (PCT) David Batenzi.
Maharusi wakiwasalimia waumini waliohudhuria ibada hiyo (hawapo pichani)
Maharusi wakionesha pete zao za ndoa muda mfupi baada ya kuvishana.
Uthibitsho wa ndoa ni vyeti vya ndoa ,na hapa maharusi wakitia saini katika vyeti vyao.
Wagebi mbalimbali walihudhuria ibada hiyo ,na hapa ni mbunge wa Viti maalum Lucy Owenya (wa kwanza)
"Mmetuona "ni kama ndio maneno yaliyokuwa vichwani mwao maharusi ,Joshua Nassari na Anande Nnko wakionesa vyeti vyao vya ndoa.
Gavana wa kwanza wa Tanzania Mzee Edwin Mtei na Mama Mtei pia walikuwa katika inada hiyo.
Wazazi wa Maharusi ,Joshua Nassari na Bi Anande Nnko.
Bw na Bi Joshua Nassari na wakiweka Sadaka zao katika kapu la sadaka.
Maharusi ,wakapata nafasi ya kusalimiana na Mzee Edwin Mtei.
Ibada ya ndoa ikawa imefika tamati na maharusi wakatoka kanisani tayari kwa msafara wa magari kuelekea uwanjani.
Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.
Mbunge Joshua Nassari na Anande Nnko wakiwa mbele ya zawadi yao ya
Ng'ombe ilitolewa na waumini wa Kanisa la Kilinga ambako ibada ya ndoa
ilifanyika,kanisa linaloongozwa na Mchungaji Babu.

Mbunge Joshua Nassari na Anande Nnko wakiteta jambo .

Baba Mzazi wa Joshua Nassari,Mzee Samwel Nassari akimpongeza mwanae kwa hata hiyo.
Mamsapu akianza majukumu ya kuhakikisha Mzee anakuwa nadhifu kila wakati.
Maharusi wakaaga katika viwanja vya Kanisa la Kilenga .
Bi Harusi Anande Nnko akiwa katika gari tayari kuelekea katika viwanja vya Usa-River Academy.
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki ,Joshua Nassari na ,Anande Nnko
wakiwa ndani ya gari muda mfupi baada ya kufunga ndoa katika kanisa la
Kilinga wilayani Arumeru tayari kwa kuelekea viwanja vya  Usa-River
Academy.

Msafara ukaanza safari ya kuelekea barabara kuu ya Moshi/Arusha ukitokea kanisani Kilinga.
Baadae maharusi wakabadili gari ili waweze kuonekana vyema na wakazi wa jimbo la Arumeru Mashariki.
Maharusi wakiwa katika gari la wazi huku wakipunga mikono kwa watu waliokuwa barabarani.
Mharusi waki "Show Love"
Kila sehemu msafara wa magari ya maharusi ulipopita ,wakazi wa maeneo hayo walionesha furaha zao .
Barabarani kulijaa watu wakimshangilia Mbune wao akijinyakulia Jiko.
Kama kawaida Jasiri haachi asili na muacha asili ni hasidi na hana akili.
Msafara wa magari ulikuwa ni mrefu .
Madereva wa boda boda pia walikuwepo kuongoza msafara .
Wananchi hawa jamii ya Maasai walitembea umbali mrefu na msafara huku wakiimba nymbo na hatimaye msafara ukaingia Ngurdoto Mountain Lodge kwa ajili ya upigaji wa picha .
Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini alikuwa katika sherehe hiyo matukio mbalimbali mtaendelea kuyapata hapa na http://dixonbusagaga.blogspot.com.