| Mhe. Membe akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Ubalozi wa Tanzania nchini China. Kulia ni Mhe. Lt. Jen. (Mstaafu) Abdulrahaman Shimbo, Balozi wa Tanzania nchini China. |
| Mhe.
Membe katika mazungumzo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na
Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Balozi Mbelwa Kairuki.
Na Mwandishi Wetu, Beijing, China
MHE.
BERNARD K. MEMBE (MB.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa amewasili nchini China tarehe 24 Februari 2014 nchini China
kwa ziara ya siku tano, na kulakiwa na Bi. Sun Baohong, Makamu
Mkurugenzi wa Masuala ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje China.
Baada
ya kuwasili Mhe. Membe alipokea taarifa ya maendeleo ya shuguli za
ubalozi kutoka kwa Lt. Jen. (Mstaafu) Abdulrahaman Shimbo, Balozi wa
Tanzania hapa China ambapo pia iligusia maeneo ambayo Mhe. Waziri
atayatembelea yaani Shenzhen na Guangzhou. Baadaye Mhe. Membe na ujumbe
wake walipata chakula cha usiku na kufanya mazungumzo na Watanzania
wanaoishi Beijing China kuhusu ziara yake na masuala mengine yahusuyo
Tanzania.
Katika
salamu zake kwa Watanzania hao ambao walijumuika na wafanyakazi wa
Ubalozi na Familia zao, Mhe. Membe alieleza baadhi ya mambo yaliomleta
kwenye ziara hii ikiwa ni pamoja na maandalizi ya ziara ya Mhe. Rais
Jakaya Mrisho Kikwete nchini hapa kufuatia mualiko wa Serikali ya
Jamhuri ya Watu wa China.
Mhe.
Membe alielezea pia nia yake na Wizara anayoiongoza ya kukuza na
kuendeleza Diplomasia ya Michezo na kusema anaamini Serikali ya China
itaridhia ombi la Tanzania la kufundisha wanamichezo thelathini wa
Kitanzania kwenye michezo mbalimbali kabla ya Mashindano ya Nchi za
Jumuiya ya Madola katikati ya mwaka huu.
Mwishoni
Mhe. Membe aliwaelezea Watanzania hao mchakato unaoendelea Tanzania wa
kupitia Katiba na hoja kuu ya Wizara ya Mambo ya Nje inayowagusa
Watanzania wengi waishio ughaibuni ya Uraia wa Nchi Mbili.
Kesho
Mhe. Membe na Ujumbe wake wanatazamia kufanya mazungumzo na Makamu wa
Rais wa China, Mawaziri wa Mambo ya Nje, Biashara na Naibu Waziri wa
Usalama kabla ya kuendelea na ziara yake kwenye Jimbo la Shenzhen na
Guangzhou.
Kwenye
ziara hii, Mhe. Membe ameongozana na Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi
wa Idara ya Asia na Australasia Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Nakuala
Senzia Mkurugenzi Kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania, Bi. Mindi Kasiga
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na maafisa waandamizi wa Wizara ya
Mambo ya Nje.
|






0 comments:
Post a Comment