SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, September 21, 2013

Wenyeviti wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF,Freeman Mbowe wa Chadema na James Mbatia wa NCCR-Mageuzi Walivyokutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema na Kukubaliana Maandamano Yaliyokuwa Yafanyike leo Yasitishwe,Mkutano Mkubwa wa Hadhara Kufanyika Jangwani Leo

 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es salaam jana kwa ajili ya mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema kuhusu mkutano wa hadhara wa kuhamasisha wananchi kuhusu mchakato wa katiba mpya, utakaofanyika leo katika viwanja vya Jangwani
  Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrajim Lipumba akiwasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.
  Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia akiwasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi
  Prof. Ibrahim Lipumba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu makubaliano yao na Jeshi la Polisi kuhusu Mkutano wao utakaofanyika leo katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam.
  IGP, Said Mwema akizungumza na waandishi wa habari.
  Karibuni uwanja ni wenu, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema akiwakaribisha viongozi wakuu wa vyama vitatu vya upinzani mbele ya waandishi ya habari mara baada ya kumaliza mazungumzo yao ofisini kwake.
 IGP, Said Mwema akiwashukuru viongozi wa vyama vya upinzani waliofika kwa mazungumzo ofisini kwake. Kushoto ni Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwenyekityi wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba akipongezana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Picha Zote na Francis Dandee

0 comments:

Post a Comment