SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, August 29, 2013

The Project for the Construction of a Two-storey Classroom Block at Enyoito Secondary School in Arusha District

H.E. Masaki Okada, the Ambassador of Japan, and Hon. Goodluck J. Ole-Medeye, Deputy Minister of Land, Housing and Human Settlements Development, attending the signing ceremony of Japanese grants at Enyoito Secondary School in Arusha District, Arusha Region. From left to right: Mr. Mwatandu Jilanga, District Education Officer,Mr. Sifael Ole-Ngushwai Mollel, Regional Cultural Officer, Hon. Nyerembe D. Munasabi, District Councilor, H.E. Masaki Okada, the Ambassador of Japan, Hon. Goodluck J. Ole-Medeye, Deputy Minister of Land, Housing and Human Settlements Development and District Council Vice Chairperson, Hon. Anna Msuya.
Signing the contract, from left to right: Mr. Gibson Meiseyeki, Oltroto Ward Councilor , Mr. Saleh Mputa Mweri, the Ag. headmaster of Enyoito Secondary School, H.E. Masaki Okada, the Ambassador of Japan and Hon. Goodluck J. Ole-Medeye, Deputy Minister of Land, Housing and Human Settlements Development
Contract is signed, from left to right: Mr. Saleh Mputa Mweri, the Ag. headmaster of Enyoito Secondary School and H.E. Masaki Okada, the Ambassador of Japan.
Ambassador Okada giving a speech. On his left are Mr. Sifael Ole-Ngushwai Mollel, Regional Cultural Officer and Hon. Nyerembe D. Munasabi, District Councilor. On his right is Hon. Goodluck J. Ole-Medeye, Deputy Minister of Land, Housing and Human Settlements Development.
Performance of Japanese traditional drum group.

The Project for the Construction of a Two-storey Classroom Block at Enyoito Secondary School in Arusha District, Arusha Region, which took place on 25 August 2013.
SOURCE: Embassy of Japan

Mchango wa ASA katika kuzalisha mbegu bora Kitaifa.

PICHA-2

Mkurugenzi wa Masoko na Usambazaji kutoka Wakala wa Mbegu za Kilimo Bw. Philemon Kawamala akieleza kwa waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam kuhusu mchango wa wakala huo katika uzalishaji wa mbegu bora za kilimo kwa kipindi cha misimu sita tangu kuanzishwa. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Bi. Zamaradi Kawawa.

IMG_3149-PICHA

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Masoko na Usambazaji kutoka Wakala wa Mbeg u za Kilimo Bw. Philemon Kawamala (hayupo pichani)(Picha na Fatma Salum-Maelezo).

Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) ulianzishwa tarehe 23 Juni, 2006 chini ya sheria ya wakala namba 30 ya mwaka 1997.

Pamoja na majukumu mengine jukukumu kubwa la wakala ni kuongeza uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora nchini.

Msimu wa kwanza  wa 2006/2007 wakala ulizalisha tani za mazao mbali mbali 429  ambapo ilikuwa ni sawa na asilimia 2.6 ya soko la mbegu nchini na hadi kufikia 2011/2012 uzalishaji umeongezeka na kufikia tani 5,542 sawa na asilimia 19.79 ya soko la mbegu nchini.

Aina Mpya ya Mpunga kwa Afrika (NERICA-series)

Kamati ya mbegu ya taifa imepitisha aina tano za mpunga wa nchi kavu aina ya AMMKA au NERICA. Kirefu cha AMMKA ni Aina mpya ya mpunga kwa Africa au kwa kiingereza NERICA”New Rice for Africa”

AMMKA  ni jina linalounganisha aina nyingi za mpunga kwenye kundi moja.

Aina hizi ni NERICA -1, NERICA-2, NERICA-4, NERICA-5 na WAB450.

Kutokana na hali ya mabadiriko ya tabia nchi na hasa ukame, aina hizi zinavumulia sana ukame na zinapandwa kwenye maeneo yanayotegemea mvua kama mahindi.

Aina hii itachangia sana katika kuongeza uzalishaji wa mpunga hapa nchini kwani maeneo kama haya ni mengi ikilinganishwa na mabonde ya umwagiliaji au mabonde yanayotegemea mvua.

Natumia fursa hii kuwaambia wakulima wa Tanzania kulima aina hizi mpya za mpunga.

Kwa wakulima wanaopata mvua za muda mrefu wana nafasi ya kupanda na kuvuna mara mbili kwa mwaka kwani zinakomaa kwa muda mfupi kwa kutumia siku 90 hadi siku 100 shambani.

Mfumo mpya  wa kuhamasisha matumizi ya mbegu bora kwa wakulima kutumia mnyororo wa thamani “ASA-APPROACH”

Mnyororo wa thamani wa zao husika huanzia upatikanaji wa pembejeo, uzalishaji, kuvuna, kuongeza thamani na kuuza kwenye masoko yaliyokusudiwa.

Mfumo wa zamani katika kuandaa teknolojia hadi kuifikisha kwa walengwa haukuwa ukiangalia sana mahitaji ya soko. Katika mfumo huu wa ASA  wakulima na wasindikaji wanapewa aina 13 za mbegu ya mpunga na kuzitathimini kuanzia upandaji, utunzaji wa shamba, uvunaji na usindikaji na mwisho wakulima kwa kushirikiana na wafanya biashara huchagua mbegu ambayo wanajua itatoa ushindani kwenye soko na mbegu hiyo huzalishwa kwa wingi ili kukidhi mahitaji yao.

Mfumo huu tulianza kuujaribu kwenye zao la mpunga na kuongeza matumizi ya mbegu kutoka tani 60 mwaka 2007 na kufikia tani 1500 mwaka 2012. Katika msimu wa 2012/13 ASA imefanyakazi na vijiji 120 katika kanda ya kati kwenye zao la alizeti ambapo tayari mwitikio kwenye matumizi ya mbegu ya alizeti unaaza kuwa mzuri ikilinganishwa na hapo awali.

Monday, August 19, 2013

Rais Jakaya Kikwete Ampongeza Dk Stergomena Tax Kwa Kuchaguliwa Kuwa Katibu Mtendaji mpya wa SADC

 Katibu Mtendaji mpya wa SADC Dr.Stergomena Tax akila kiapo mbele ya jaji mkuu wa Malawi Anastazia Msoza wakati wa mkutano wa 33 wa wakuu wa nchi za SADC uliofanyika jijini Lilongwe Malawi  jana
  Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza katibu Mtendaji mpya wa SADC Dkt.Stergomena Tax wakati wa kikao cha 33 cha wakuu wa nchi za SADC kilichofanyika jijini Lllongwe Malawi jana kikao hicho kimeisha jana. Kushoto ni Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
 Rais wa Malawi,  Dkt. Joyce Banda (wa pili kushoto) na Jaji Mkuu wa ,Malawi, Anastazia Msosa, na Dkt. Nkosazana Dlamini Zuma (kulia) wakimpongeza Dkt. Tax, baada ya kutangazwa kushika nafasi hiyo  jana
Rais wa  Dkt. Joyce Banda(wa pili kushoto) Jaji Mkuu wa Malawi Mhe. Anastazia Msosa,na Mwenyekiti wa Umoja wa Africa (AU) Dkt. Nkosazana Dlamini Zuma wakimpongeza  katibu Mtendaji mpya wa SADC Dkt.Stergomena Tax baada ya kula kiapo wakati wa kikao cha 33 cha wakuu wa nchi za SADC kilichofanyika jijini Lllongwe Malawi. Picha na Mdau Freddy Maro-IKULU

Mikutano ya Mabaraza Huru ya Katiba Mpya Kutoka Chadema

 Katibu Mkuu wa Cahdema Dk.Wilbrod Slaa akihutubia mkutano-kiomboi.
  Sehemu ya maelfu ya wakazi wa mji wa Muleba mkoani Kagera, wakiwa katika mkutano wa hadhara wa Mabaraza ya Wazi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ya kujadili rasimu ya katiba mpya, uliofanyika kwenye Uwanja wa Red Cross pichani wakimsiliza Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe
 Sanjenti mstaafu akitoa maoni Kiomboi-Singida.
Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU), wakiwa wamevalia nguo za kimapambano wakati wakilinda mkutano wa Mabaraza Huru ya Katiba Mpya, uliohutubiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willbrod Slaa katika eneo la Kiomboi, Wilaya ya Iramba, Singida.
Na Mpiga Picha wetu na Joseph Sanga

HUDUMA YA MAWASILIANO YA VODACOM YAREJEA KAMA KAWAIDA

Baada ya kukosekana kwa huduma za mtandao wa Vodacom kwa takribani masaa 16, huduma hizo zimerejeshwa katika hali yake ya kawaida asubuhi  ya Jumamosi ya Agosti 17.
 
Akizungumzia tatizo lililosababisha kukosekana kwa huduma za mawasiliano kwa watumiaji wa mtandao huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Rene Meza (pichani juu) amesema chanzo cha kukatika kwa mawasiliano nchi nzima siku ya Ijumaa ni moto uliotokea katika mtambo mkuu wa kuendeshea mtandao (Main Switch) uliyoko Dar es Salaam.

 “Kufuatia hatua hiyo, hatukuwa tena na uwezo wa kutoa huduma kwa watu wote kuanzia siku ya Ijumaa jioni hadi Jumamosi asubuhi, hali hii iliathiri wateja wetu wote kwa ujumla kwani walishindwa kuwasiliana na ndugu jamaa na marafiki ambao wote ni wateja wetu, alisema Meza.


Aidha aliomba radhi kwa jamii ya Watanzania na wateja wa Mtandao wa Vodacom kwa kukosa mawasiliano katika kipindi hicho, na kusema kuwa wateja wote wa mtandao wa Vodacom watarudishiwa gharama zote kwa huduma yoyote walionunua na kuhitaji kuitumia wakati ambapo mtandao  haukuwa unapatikana, “Fidia hizi kwa wateja wetu wote zitatolewa siku ya jumatatu ya Agosti 19, 2013 alisema Meza.

 “Tunaishi katika dunia ambayo mawasiliano ni muhimu katika maisha yetu ya kila siku hivyo tunaelewa kuwa tatizo hili limekuwa kikwazo kikubwa kwa wateja wetu, Na tunawashukuru kwa kuwa waelewa na wavumilivu katika kipindi chote ambacho tumekuwa tukikabiliana na tatizo hili, alisema Meza.

Meza alihitimisha kwa kuhakakikishia Watanzania na wateja wa Vodacom kwa ujumla kuwa Vodacom imedhamiria kuendelea kutoa huduma zenye viwango vya hali ya juu nchini.

 “Ninapenda kuwashukuru wafanyakazi wetu wote na washirika wetu ambao kwa pamoja wamefanya kazi bila kuchoka katika kuhakikisha huduma zote zinarejea hadi katika hali ya kawaida hadi kufikia Jumamosi asubuhi, Jitihada zao na kazi kubwa waliyoifanya imewezesha huduma zote kurejea katika hali ya kawaida, alihitimisha Meza.
 CHANZO-HAKINGOWI

Rais wa Zanzibar Dr Ali Shein Ashiriki Maziko ya Mtumishi wa Chama cham ASP na CCM Mzee Ased Ramadhan Mjini Unguja

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,akitia udongo katika kaburi la Marehemu Mzee Ased Ramadhan.  Marehemu alikuwa Mtumishi wa Chama cham ASP na CCM,ambapo alishika nafasi mbali mbali zikiwemo Mkuu wa Utawala Makao Makuu ya ASP na Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja jana. 
  Baadhi ya Wananchi walioshiriki mazishi ya Marehemu Mzee Ased Ramadhan wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu huyo Aliyefariki jana na kuzikwa katika makaburi ya Mwanakwerekwe mjini Unguja jana.marehemu aliwahi kushika nyadhifa mbali mbali katika Chama cha ASP na CCM.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa na viongozi wengine wa Serikali wakati wa kumswalia  Marehemu Mzee Ased Ramadhan. Marehemu alikuwa Mtumishi wa Chama cham ASP na CCM,ambapo alishika nafasi mbali mbali zikiwemo Mkuu wa Utawala Makao Makuu ya ASP na Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja jana.
Picha na Ramadhan Othman,IKULU-Zanzibar