SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, April 5, 2013

UCHAGUZI WA WAJUMBE WA KATIBA NGAZI ZA MTAA WAFANYIKA OYSTREBAY JIJINI DAR

Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam, wakiwasikiliza baadhi ya wagombea hawapo (pichani) wa nafasi za ujumbe wa uwakilishi wa baraza la Marekebisho ya Katiba  yaliyofanyika katika Mtaa huo uliopo Kata ya Msasani jijini Dar es Salaam.

Wagombea wa nafasi za ujumbe wa baraza la Marekebisho ya Katiba  kutoka  Mtaa wa Oysterbay Kata ya Msasani jijini Dar es Salaam, wakipiga kura wakati wa uchaguzi huo uliofanyika jana katika shule ya msingi Oysterbay, kutoka kulia ni Eustace Mtumbuka, Bujiku Sakila, Amos Mwakilasa, Wilfred Mpembe, Anna Matinde na Charles Igogo  ambao walichuana katika nafasi za jumla katika kundi hilo Charles Igogo na Bujiku Sakila waliibuka washindi.
Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Oysterbay jijini Dar es Salaam, wakiwa katika uchaguzi wa nafasi za ujumbe wa uwakilishi wa baraza la Marekebisho ya Katiba  yaliyofanyika katika Mtaa huo uliopo Kata ya Msasani jijini Dar es Salaam.
Msimamizi wa uchaguzi katika Mtaa wa Oysterbay  akitangaza matokeo ya uchaguzi wa nafasi za ujumbe wa uwakilishi wa baraza la Marekebisho ya Katiba  yaliyofanyika katika Mtaa huo uliopo Kata 
CHANZO: NA GPL

0 comments:

Post a Comment