SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, October 9, 2012

Mwekezaji Kwenye UDA, Simon Group LTD ‘Amwaga’ Mabasi 15 Awamu ya Kwanza

PictureViongozi wa Kampuni ya Simon Group na wengine Wakielekea kuzindua mabasi15 waliyowekeza UDA.
Picture
Habari na Elias Msuya via gazeti la Mwananchi ---  KAMPUNI ya Usafiri jijini Dar es Salaam (UDA) imejipanga kuteka soko la usafiri nchini ifikapo mwezi Machi mwaka 2013.

Picture
Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group,Robert Kisena (wa pili kulia) Wawekezaji wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA akipokea mfano wa funguo kutoka kwa Meneja wa Biashara wa TATA Afrika Holding Tanzania Ltd,Srinivas Nemalapuri (wa pili kushoto) kulia ni Mkurugenzi wa Simon Group, Leonard Rubuye na kushoto Kaimu Meneja Biashara,Sarvan Keshri. ikiwa ishara makabidhiano ya mabasi 15 katika awamu ya kwanza, hafla hiyo ilifanyika kwenye Ofisi za UDA Dar es Salaam.
Picture
Mwenyekiti Mtendaji wa Simon Group,Robert Kisena (wa nne kushoto) akiwaongoza viongozi wengine ndani ya Basi la UDA.
===
Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena alipokuwa akipokea mabasi 15 kutoka kampuni ya Tata Africa ya India ikiwa ni sehemu ya mabasi 30 yanayotarajiwa kuingizwa nchini ifikapo Desemba mwaka huu.

Kisena alisema kampuni ya Simon Group iliyowekeza katika shirika la UDA imejipanga kuwa kampuni kubwa barani Afrika kwa mtaji wa Dola25 milioni (sawa na Sh375 bilioni)  utakaowezesha kupatikana kwa mabasi 300 ifikapo mwezi Machi mwakani, “Simon Group imejipanga kuwa kampuni kubwa Afrika ifikapo Machi mwakani na tuna mpango wa kununua mabasi 300 kwa mtaji wa Dola25 milioni,” alisema Kisena.

Aliongeza kuwa kati ya mabasi hayo kutakuwa na mabasi ya wanawake, mabasi ya wanafunzi, mabasi ya binafsi, mabasi ya mikoani na mabasi yatakayosafiri barani Afrika, “Mazingira mabovu ya sasa ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam mara kwa mara yamekuwa yakisababisha udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake, bila shaka wengi wenu mtakumbuka vizuri kisa cha Maumba. Tunataka kukomesha udhalilishaji huo kwa wanawake ili wasafiri kwa uhuru na raha mstarehe,” alisema Kisena.

Kuhusu mabasi ya wanafunzi, alisema yatakuwa matano kila barabara kuu jijini Dar es Salaam na yatafanya kazi hiyo tu.

Kuhusu mabasi ya binafsi (Executive class), alisema yatakuwa na nauli ya juu lakini yatatoa huduma kama vile televisheni, vinywaji, magazeti na kiyoyozi, “Tunataka tuwahamasishe watu wasitumie tena magari yao binafsi. Unajua kwa mwezi mtu hutumia katiya Sh800,000 hadi Sh1milioni kununua mafuta ya gari, hela ambayo ni nyingi mno. Lakini kwa kutumia usafiri huu, inawezekana kubana matumizi,” alisema.

Akizungumzia mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) alisema kuwa wanatarajia kushinda zabuni ya kuuendesha kwa kuwa kampuni hiyo haina mshindani katika usafirishaji nchini, “Kwa sasa Dart inajengwa barabara ya Morogoro na barabara itakamilika mwaka 2014. Kwa sasa tutaendesha mradi huo kabla Dart haijaanza na kwa barabara nyingine baada ya hapo. Kwa kuwa sasa UDA haina mpinzani katika sekta ya usafirishaji nchini, naamini tutashinda zabuni ya kuendesha,” alisema. Aliongeza kuwa mradi huo unatarajia kutoa ajira kwa zaidi ya Watanzania 1,500.


CHANZO: BOFYA

0 comments:

Post a Comment