SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, October 10, 2011

AIRTEL YAKABIDHI CHEREHANI 10 KWA YATIMA IRINGA

Kulia ni Meneja wa Kanda ya Kusini  wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel,  Fredrick Mwakitwange akimkabidhi bwana Geoff Fox  (kushoto) moja ya cherehani kati ya vyerehani 10 vilivootolewa msaada kwa ajili ya kituo cha kulea na kusomesha watoto yatima  kinachojulikana kama Mufindi Orphans (Fox farm) kilichopo Iringa. Kituo hiki kinatunza watoto 56 na kusaidia zaidi ya watoto 1200 wa vijiji vya jirani,  nyuma yao ni  baadhi ya watoto wa kituo hicho, wafanyakazi wa Airtel na wafanyakazi wa kituo hicho wakishuhudia makabidhiano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki.
 
Picha maalum inayoashiria shukrani maalum kwa Airtel iliyoandaliwa kwa ubunifu wa watoto wa kituo cha Mufindi Fox wakati Airtel ilipotoa msaada wa cherehani 10 kwa kituo hicho kinacholea watoto yatima 56 kilichopo mkoani Iringa.
***************
Press Release
Airtel yatoa msaada wa cherehani 10 kwa kikundi cha kulea watoto Yatima mkoani Iringa
Oktoba 9, 2011, Kampuni ya simu za mikononi ya AIRTEL imetoa msaada wa vyerehani kumi  kwa kikundi  kinacholea watoto yatima mkoni Iringa ili kukiongezea uwezo wa  kupambana na changamoto zinazokikumba
Msaada huo umekabidhiwa na meneja wa Kanda ya Kusini wa airtel Fredrick Mwakitwange kwa kikundi hicho kinacholea na kufundisha watoto yatima Iringa kijulikanacho kama Mufindi Orphans (Fox farm) chenye watoto 56 ndani ya kituo pamoja na kufundisha zaidi ya watoto 1200 wa vijiji vya jirani
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Meneja wa Kanda ya Kusini wa Airtel Bw Fredriki Mwakitwange alisema “AIRTEL tutaendelea kugawa  misaada kwa vikundi vya wasiojiweza ikiwa ni sehemu ya kampeni yatu ya kusaidia jamii katika kutatua baadhi ya matatizo ambayo yanayakabili”.
Airtel tunaguswa sana na matatizo yanayowakabili watu mbali mbali katika jamii ikiwa ni pamoja na matatizo ya MUFINDI Orphans (Fox Farm) na tunaamini mashine hizi zitawasaidia kuanzisha mradi endelevu ambao utawasaidia kujitengenezea kipato ambacho kitawasaidia w watoto hawa kuweza kupata chakula, malazi, mavazi pamoja na elimu.
Airtel kwa kutambua umuhimu wa kusaidia jamii Misaada yetu bado tutaendelea kuielekeza kwenye sekta za Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii  kama tunavyofanya leo hapa Iringa
Akipokea msaada huo wa mashine za kushonea, Mlezi wa  kikundi cha Mufindi Orphans, Kituo cha  kulelea watoto yatima Bw Geoff Fox alisema  “ Msaada huu  utatusaidia katika kuboresha utoaji wa huduma kwa watoto hawa. tunachangamoto nyingi ikiwemo idadi kubwa ya watoto na kipato kidogo cha uendeshaji, hivyo tunawapongeza sana Airtel kwa kushirikiana nasi katika kusaidia jamii.
Kupitia cherehani hizi tutaanzisha madarasa ya ushonaji na ada zitakazolipwa zitatumika kusaidia watoto hawa, vilevile chereharani zitatumika kushona vitambaa na mashuka ambayo yatatumiwa na watoto pia yataleta pato katika kikundi na tutaweza hata kuendelea kuwasomesha watoto hawa vizuri” aliendelea kusema Bw Geoff Fox
Airtel imekuwa mstari katika kusaidia uboreshaji wa maisha ya jamii kwa   kutoa misaada ya aina mbalimbali na kudhamini shughuli za miradi ya maendeleo.Mwezi uliopita licha ya kutoa misaada ya vitabu kwa shule za sekondari mikoa ya Tanga, Moshi na Arusha pia ilitoa msaada wa cherehani 10 kwa vikundi vitatu vya kulea watoto yatima  jijini Dar es salaam ikiwa ni pamoja na kikundi cha wanawake cha Msasani,kikundi cha Huruma cha Kawe pamoja na kile cha kulea watoto yatima cha Kinondoni.
Watoto wanaolelewa katika vituo hivyo vya Dar es salaam na Iringa cha Mufindi Fox  bado wanamahitaji mengi japo kampuni ya simu za mkononi airtel imeweza kujitolea msaada huo wa vyerehani bado pia wanahitaji ya vifaa vya shule, vifaa vya kujifunzia, chakula pamoja na malazi ya kila siku
Mwisho.

0 comments:

Post a Comment