SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, June 9, 2011

BHOKE AWATAKA WATANZANIA WASIKATE TAMAA KUSHIRIKI BIG BROTHER!!

Mwakilishi wa Tanzania Big Brother Amplified Bhoke Egina (katikati), Kulia ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Bi. Furaha Sumalu na Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi.
Barbara Kambogi akiwasisitiza Watanzania waendelee kupiga kura Big Brother Amplified japokuwa Tanzania haina mwakilishi. Kulia Bhoke Egina.

Bhoke Egina akishow love na Mdau Othman Michuzi.
The Multichoice Sisters Barbara Kambogi na Furaha Sumalu. “Welcome Back Home”.
****************************************
Watanzania wametakiwa kutokuwa na mtazamo hasi dhidi ya washiriki pamoja na shindano la Big Brother na badala yake wawaunge mkono kwa kuwa lile ni shindano kama menginena zaidi linemjengea mshiriki ujasiri na kujitambua.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, mmoja wa waliokuwa wawakilishi wawili wa  Tanzania katika shindano la mwaka huu la Big Brother Amplified Bhoke Egina amesema ushiriki wake umemsaidia kujifunza mengi ikiwa ni pamoja na kumpa uwezo wa kusoma tabia za watu tofauti na namna ya kuishi nao na pia kujua uwezo wake mwenyewe wa uvumilivu na kiwango cha ujasiri.
Mwakilishi huyo ambaye alitolewa katika jumba hilo kwa kura Jumapili iliyopita alionesha umahiri wake alipokuwa ndani ya shindano hilo, kwa kuweza kumudu kukaa kwa wiki tano akiishi na washiriki wengine 26 kutoka mataifa mbali mbali ya Afrika wakiwemo wa kutoka nchi jirani za Kenya na Uganda.
Bhoke ni mwakilishi wa pili kutoka Tanzania kutolewa katika mashindano hayo, baada ya mwakilishi mwingine Lotus Kyamba kuenguliwa takriban majuma mawili yaliyopita kwa kuvunja sheria za ndani ya mjengo huo, kufuatia kumnasa kibao mwakilishi kutoka Afrika Kusini baada ya kutofautiana kimitazamo.
Naye Meneja Uhusiano wa Multi Choice Tanzania Barbara Kambogi amesisitiza umuhimu wa watanzania kuendelea kuwapigia kura washiriki waliobaki ndani ya jumba hilo, japokuwa Tanzania haina mwakilishi kwa sasa, ili kuwezesha kufanikisha shindano hilo hadi hatua ya kupatikana kwa mshindi.
Amesema kwa sasa upigaji kura ni rahisi, akisema njia ya kwanza ni kwa kutumia simu ya mkononi kwa mitandao yote isipokuwa ‘airtel’ ambapo unatuma ujumbe wa maandishi kwa kuandika neno VOTE kisha jina la mshiriki unayetaka abaki na unatuma kwenda namba 15726 na njia ya pili ni kwa kutumia mtandao, ambapo kuna website ya Big Brother ambayo ni www.mnetafrica.com/bigbrother ikiingia utaona maelekezo ya jinsi unavyoweza kupiga kura.
Na mo Blog

0 comments:

Post a Comment