SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, February 22, 2011

TANZANIAN STUDENTS ASSOCIATION OF HYDERABAD (TSAH)
Ndugu Watanzania, tarehe 27 February 2011, jumapili, kutakua na mkutano wa wana-TSAH, utakaofanyika nyumbani kwa Dany Msemo, Yaprar,Sainkpur, kuanzia saa tisa na nusu alasiri.
Tunaombwa kufika bila kukosa kwa ajili ya ufafanuzi wa mambo kadhaa yaliyojitokeza.
Pia, kikao hicho kitajadili mambo mbalimbali yanayohusu jumuiya yetu.
Mbali na hayo, ijulikane wazi kuwa, Katibu mkuu wa TSAH amepokea barua ya kujiuzulu kwa Mwenyekiti wa TSAH, na Makamu wake.
Mamlaka husika ndio inaweza kukubali wajiuzulu au kukataa kujiuzulu kwao baada ya kujiridhisha na maombi hayo.
Tunaombwa kufika wote bila kukosa.
Uwepo wako ni mhimu sana katika uimarishaji wa jumuiya yetu TSAH.
Katibu Mkuu TSAH
John Gagah
+91 950 26 96 870
jonbalele@gmail.com

0 comments:

Post a Comment