TAMASHA DOGO LA ZIFF 31- Dec – 2010 NGOME KONGWE.
TAMASHA dogo la Zanzibar International Film Festival (ZIFF) ambalo
limepewa jina la ZIFF Min ZIFF lipo tayari kufanyika baada ya kutangaza
filamu zitakazoonyeshwa katika tamasha hilo, Mini-Festival
itakayofanyika Ngome Kongwe, Zanzibar kuanzia tarehe 31/12/2010 hadi
2/01/2011, itakua ni Tamasha dogo la siku 3 katika kutoa muamko kwa
Tamasha kubwa la ZIFF lijalo (2-10 Julai, 2011).
Tamasha hili dogo litajumuisha filamu za kitanzania pekee yake (Swahili Films) ili kuendelea kutoa mwamko kwa watengenezaji filamu wa Tanzania kufanya vyema katika tasnia hii, Tamasha hili litaonyesha filamu 8 za Kitanzania na filamu 2 bora kati ya hizo zitaenda kuoneshwa katika Tamasha kubwa la filamu Afrika – FESPACO huko Burkina Faso.
Tamasha hili dogo litajumuisha filamu za kitanzania pekee yake (Swahili Films) ili kuendelea kutoa mwamko kwa watengenezaji filamu wa Tanzania kufanya vyema katika tasnia hii, Tamasha hili litaonyesha filamu 8 za Kitanzania na filamu 2 bora kati ya hizo zitaenda kuoneshwa katika Tamasha kubwa la filamu Afrika – FESPACO huko Burkina Faso.
Filamu hizo ni Best Wife, Don’t Cry, Briefcase, Huba, Divorce, This
is it, Nani, na Black Sunday, mbili kati ya filamu hizi ndiyo
zitakazochaguliwa na kuingia kwenye maonyesho ya filamu makubwa Afrika –
FESPACO nchini Burkina Faso.
Kama ilivyo ada ya Tamasha la Filamu la Nchi za Majahazi, kutakuwa
pia na makundi ya muziki na wakati huu kundi zima la THT litafanya
maonyesho kwa siku zote tatu, watakao kuwepo ni Mwasiti, Marlaw,
Mataluma, Amin, Barnaba, Pipi, THT Dancers na wengineo. Kwa habari
zaidi tembelea www.ziff.or.tz
Tamasha la ZIFF limekuwa na mafanikio makubwa kimataifa mwaka huu.
Tarehe 3-5 Decemba ZIFF ilionyesha filamu zake huko Potsdam Ujerumani
ambako mtengenezaji filamu Sajani Srivastava alionyesha filamu ya
Tanzania “Nani” ambayo iliwafurahisha sana watazamaji.ZIFF pia
ilionyesha filamu zake katika tamasha la Trinidad and Tobago na pia
inatarajia kuonyesha filamu zake huko New york African Art Museum mwaka
ujao.
Tayari matayarisho ya Tamasha la 14 yameanza na kwa sasa kuna uhakika
wa kuwa na Workshop juu ya utengenezaji filamu itakayoendeshwa na
Deustsche Welle ya ujerumani.
Kwa upande wa Muziki Clouds Entertainment wameingia mkataba na ZIFF kuendesha shughuli za muziki katika ZIFF.




0 comments:
Post a Comment