SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, September 10, 2010

Ripoti: Askari wa Israel wawabaka watoto wa Kipalestina wanaowakamata

 Sample Image
Ripoti ya uchunguzi iliyotolewa hivi karibuni na mtandao wa Ynet imesema askari jeshi wa utawala haramu wa Israel wamekuwa wakiwabaka watoto wadogo wa Kipalestina wanaowakamata. Ripoti hiyo imesema kuwa, watoto 5 Wapalestina ni miongoni mwa watoto wengi ambao wametiwa mbaroni na askari hao pasina kufunguliwa mashtaka kwa makosa madogo madogo yanayowakabili kama vile ya kurusha mawe. Aidha, ripoti hiyo imebainisha kuwa askari hao wamekuwa wakiwalawiti na kuwatesa vijana wadogo wa kiume ambao wamezuiliwa katika vituo vya utawala wa Israel. Ukiukaji huo wa haki za watoto umekuwa ukilaaniwa na jamii ya kimataifa lakini Israel imekuwa ikiendelea kuwazuilia hata watoto walio chini ya umri wa miaka 14.

0 comments:

Post a Comment