
Polisi ya China imeripoti kuwa idadi ya watu waliofariki dunia kwenye maporomoko ya udongo mkoani Yunnan nchini humo imefikia 38 huku wengine zaidi ya 54 wakitoweka. Shirika la Habari nchini humo la Xinhua limesema kuwa, timu ya waokoaji imeweza kuokoa mwili wa mtu mmoja tu hadi kufikia sasa kwenye vifusi vya majengo yaliyofukiwa na udongo kufuatia maporomoko hayo. Licha ya serikali ya China kujaribu kutengeneza daraja linalounganisha eneo la janga na eneo ambalo halijaathirika, vijiji vilivyoko katika mkoa huo wa Yunnan vimeendelea kuathirika pakubwa na mafuriko pamoja na maporomoko. Janga hilo la kimaumbile la mvua kubwa limeikumba China tangu mwishoni mwa mwezi Mei na kusababisha mafuriko na maporomoko ambayo yamepelekea mamia ya watu kupoteza maisha yao.




0 comments:
Post a Comment