SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, July 10, 2010

DR.SHEIN AIBUKA KINARA KINYAG'ANYIRO CHA KUWANIA KUGOMBEA URAIS KISIWANI ZANZIBAR
HATIMAYE MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANAZANIA DR. ALLY MOHAMED SHEIN AMEIBUKA KIDEDEA KWA KURA 117 NA KUWABWAGA WAPIZANI WAKE DR. GHALIB BILAL NA WAZIRI KIONGOZI WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR SHAMSI VUAI NAHODHA KATIKA KINYAG'ANYIRO CHA KUWANIA KUGOMBEA URAIS KISIWANI ZANZIBAR.
DR.SHEIN ALIWASHINDA GHALIB BILAL AMBAYE AMEPATA 54 NA KUSHIKA NAFASI PILI AKIFUATIWA NA SHAMSI VUAI NAHODHA AMBAYE AMESHIKA NAFASI YA TATU KWA KUPATA KURA 33.
Ushindi wa Dr Shein na matukio mbali mbali ya mkutano wa kamati kuu.
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dr.Ali Mohamed Shein akiwashukuru wajumbe wa Halmashauri kuu ya taifa CCM kwa kumchagua kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM.
Mwanasiasa Mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru akimpongeza Dr.Gharib Bilal kwa kukubali matokeo ya uchaguzi ambapo Dr.Ali Mohamed Shein aliibuka mshindi katika ugombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM jana usiku mjini Dodoma.
Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao maalumu cha Halmshauri kuu ya CCM mjini Dodoma jana usiku.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza makamu wa Rais Dr.Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa na wajumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa CCM kuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi katika ukumbi wa White house mjini Dodoma jana usiku.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Dr.Gharib Bilal kwa kukubali matokeo ya ushindi wa Dr.Ali Mohamed Shein kuwania urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM jana usiku.
Baadhi ya wajumbe wa halmashauri kuu ya Taifa CCM wakiwa katika kikao maalum kilichompitisha Dr.Ali Mohamed Shein kuwa mgombea wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi jana usiku mjini Dodoma. (Picha na Ferdy Maro).
*****************************

MKUTANO MKUU WA CCM LIVE TOKA DODOMA SASA

MWENYEKITI WA CCM JAKAYA MRISHO KIKWETE AKIONGOZA MKUTANO MKUU WA CCM HIVI SASA HUKO DODOMA. FUATILIA MAMBO YOTE LIVE: BOFYA HAPA

0 comments:

Post a Comment