Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia jambo na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Dkt. Ali Mohamed Shein wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika leo kwenye Uwanja wa Aman mjini humo.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, akipunga mkono kwa waandamanaji waliokuwa wakipita mbele ya jukwaa kuu wakati wa maadhimisho ya sherehe za miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika leo Uwanja wa Aman mjini Zanzibar .



