SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, April 14, 2014

Man City yapata pigo kwa Yaya Toure




KLABU ya Manchester City imepata pigo baada ya kufahamika kuwa huenda kiungo wake mahiri Yaya Toure asicheze tena msimu huu baada ya kuumia katika mchezo dhidi ya Liverpool uliochezwa mwishoni mwa wiki katika Uwanja wa Anfield. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alitolewa nje wakati wa kipindi kwanza na kusababisha hali kuwa mbaya kwa kikosi chake na kupelekea kufungwa mabao 3-2 na mahasimu wao hao katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu. 

Akihojiwa kuhusiana na hali ya nyota huyo, kocha wa City Manuel Pellegrini amesema itakuwa ngumu kwa mchezaji huyo kumaliza msimu huu. 

Toure alijiumiza mwenyewe baada ya kupiga shuti lililopaa katika mchezo huo wakati City wakijaribu kurejea baada ya kufungwa bao la kuongoza na Raheem Sterling

====

Lyon yaidonyoa PSG kimoja Ufaransa

Mfungaji wa bao pekee la Lyon, Ferri (12) akipambana uwanjani dhidi ya PSG jana


MABINGWA watetezi wa Ligi ya Ufaransa, PSG jana ilionja kipigo chake cha kwanza baada ya mfululizo wa ushindi katika ligi hiyo kwa kudonyolewa goli 1-0 dhidi ya Olympique Lyon.
Ikicheza ugenini, PSG ilishindwa kufuruka kwa Lyon waliopata bao lao katika dakika ya 31 kupitia kwa Jordan Ferri.
Pamoja na kwamba kipigo hicho hakijaiteteresha matajiri hao wa Paris, lakini imefanya pengo la pointi baina ya wapinzani wanaowafukuzia kileleni, Monaco kuwa pointi 10 badala ya 13 ya awali baada ya Monaco kupata ushindi ugenini siku ya Jumamosi dhidi ya Rennes.
PSG imeendelea kusaliwa na pointi zake 79, huku Monaco wakiwa nafasi ya pili na pointi zao 69 huku timu zote zikiwa zimecheza michezo 33 na kusaliwa na mechi tano kabla ya kufungia msimu wa 2013-2014.