SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, January 29, 2014

WAFANYAKAZI WA BENKI YA CRDB WATOA SADAKA KANISA LA KKKT USHARIKA WA MSASANI


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB akizungumza na waandishi wa habari baada ya ibada ya shukrani iliyowashirikisha wafanyakazi wa benki hiyo katikaKanisa la KKKT Usharika wa Msasani.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa  la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani, Mchungaji Metili Olteshi akiongoza Ibada ya shukrani ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Waimbaji wa Kwaya ya Vijana ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani wakiimba nyimbo za kumsifu Mungu wakati wa ibada ya shukrani, ambapo wafanyakazi wa Benki ya CRDB walitoa sadaka katika kanisa hilo.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB pamoja na familia zao wakiwa katika ibada ya shukrani katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB,Tully Mwambapa akiwa katika ibada hiyo.
Kwaya ya Vijana ikiimba nyimbo za kumsifu mungu.
Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu (kushoto) akiwa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa benki hiyo, Willy ,Kamwela.
Baadhi ya maofisa wa benki ya CRDB.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa  la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani, Mchungaji Metili Olteshi akiongoza ibada.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa  la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani, Mchungaji Metili Olteshi akitoa baraka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei ma mkewe wakati wa Ibada maalumu kwa ajili ya kutoa shukrani.
Ibada ikiendelea.
Mbuzi akisubiri kupigwa mnada wakati wa ibada hiyo.
Uongozi wa juu wa Benki ya CRDB ukiwa katika picha ya pamoja na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa  la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Msasani, Mchungaji Metili Olteshi. 
Uongozi wa juu wa Benki ya CRDB ukiwa katika picha ya pamoja na mama Mzazi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Dk. Alex Malasusa (wa tano kushoto), wakati wa ibada ya shukrani.
Wakurugeniz wa Benki ya CRDB Makao Makuu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kushiriki ibabada ya shukrani.
Mameneja wa Benki ya CRDB Makao Makuu wakiwa katika picha ya pamoja. 
Wakurugenzi wa Benki ya CRDB wakiwa katika picha ya mapoja na watoto.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakiwa na familia zao.
Kwaya ya Ukombozi ikiwa katika picha ya pamoja.
Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika picha ya pamoja.

0 comments:

Post a Comment