SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, July 20, 2010

KUTOKA UDOSINI: Idadi ya watu waliofariki kwenye ajali mbaya ya treni nchini India imeongezeka


Idadi ya watu waliofariki kwenye ajali mbaya ya treni nchini India imeongezeka na kufikia 61. Idadi hiyo ambayo mchana wa leo ilikuwa imetajwa kuwa 48. 

Watu waliofariki kwenye ajali mbaya ya treni nchini India imepanda na kufikia 61. Idadi hiyo ambayo mchana wa leo ilikuwa imetajwa kuwa 48 imepanda baada ya majeruhi kadhaa kufariki wakiwa hospitalini. Zaidi ya watu 50 pia wamejeruhiwa kwenye ajali hiyo. Afisa mmoja wa serikali ya India amesema ajali hiyo ilitokea baada ya treni ya abiria kugonga treni nyingine iliyokuwa imesimama katika mji wa Sainthia kwenye jimbo la Bengal Magharibi. Duru za shirika la reli la India zinasema kuwa ajali hiyo imesababishwa na kutowajibika kwa makandawala wa magarimoshi hayo.
Hali ndio hii ilivyokuwa katika eneo la ajali .
Askari wa India wakishuhulika na kuweka Usalama katika Eneo la Ajali
Hii ndio hali halisi nchini India kwa kweli inasikitisha

0 comments:

Post a Comment