![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_ltXlMQ0SNFgAVYUT-HX3s89UdNL2PYIPtwmdodxz0YEULxdYHCI2_VpbU8uyAtTkgKzQL-xovqApBogd8UfC4ByvKD68_4laCGV_gLcQxPFSIlf3jTa3cJSq4kSCdIQbIyzYgWaVJmVP/s400/kijana+1.jpg)
Kijana Pascal
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhni0_wgUoRl7nAdjwHN393vQyNrb8-3zSa9VN4jOCUtVcbCMjbk8oR6fanE5QodZiG9k0GmYRi1SZp5SfGy_IMOykz5Dq5sstpuO02UUtNVKQP47hcaLabjHMfLtzFG1W_RP0hXaB20vcm/s400/kijana+2.jpg)
Hii ni Sehemu inayoonyesha mfupa huo wa ziada unaoendelea kukua na kumsababishia maumivu makali.
Kijana
Pascal Issa mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam ameomba msaada wa
fedha au matibabu kwa ajili ya upasuaji wa mguu wake wa kulia wenye
mifupa miwili, Kijana huyo aliyefika katika Ofisi za MO BLOG jijini Dar
es Salaam.
Aidha
Kijana huyo amewaomba wasamaria wema kumsaidia ili aondokane na mateso
anayoyapata hususani wakati wa usiku ambapo mfupa huo wa ziada
ulioanza kujitokeza tangu akiwa na umri miaka 7 mpaka sasa akiwa na
miaka 24 kuendelea kukua bila matumaini ya kupata matibabu.
Kwa yoyote atakayeguswa na tatizo la kijana huyo awasiliane naye kwa namba +255657069870 au awasiliane na Meneja wa MO BLOG kwa namba +255714940992 kwa ajili ya mawasiliano zaidi.
MO BLOG inawaomba wadau wanaoweza kumsaidia hata kupata Daktari wa kumtibu kwani kutoa ni moyo na hujafa hujaumbika.
0 comments:
Post a Comment