Meneja
wa Vodacom Tanzania kanda ya Zanzibar Mohamed Mansour kulia
akimkabidhi Tunzo Mwanamziki bora wa kiume wa nyimbo za kizazi kipya
Juma Twenty kwenye Zanzibar Music Award,zilizofanyika juzi mjini
Zanzibar na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Mbunge
wa Jimbo la Uzini Zanzibar na Mkurugenzi wa Zanzibar Media Corporation
Seif Khatibu kulia akiwa kwenye picha ya pamoja na mshindi bora wa kike
wa nyimbo za asilia Sada Mohamed mara baada ya kumkabidhi tunzo yake
kwenye Zanzibar Music Award zilizofanyika juzi mjini Zanzibar na
kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Mjumbe
wa NEC Aisha Kigoda kulia akimkabidhi Tunzo msani bora chipukizi wa
kike Sauna G kwenye Zanzibar Music Award zilizofanyika mjini Zanzibar
na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Aaah tamaduni zetu za mwambao hatuziachi kata kidogo kwenye Zanzibar Music Award tunaburudisha.
Baadhi ya masharobaroz walioudhuria Zanzibar Music Award.
Mwanamziki wa kizazi kipya Baby J akionyesha Tunzo yake ya pili mara baada ya kukabidhiwa na Meneja wa Zenj Fm.
0 comments:
Post a Comment