SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, January 14, 2011


WASANII WAFURAHIA TUZO ZA FC
WASANII mahiri katika tasnia ya filamu hapa nchini Tanzania leo hii asubuhi wameonyesha furaha kubwa baada ya kupokea tuzo hizo za Bora za 2010 zilizofanyika katika ukumbi wa Tamal Hotel uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam, wakiongea kwa nyakati tofauti wasanii hao wameupongeza mtanda huu kwa kuwajali na kuwapa moyo kwa kazi wanazofanya na kupokelewa na jamii.

“Napenda sana kuwapongeza sana filamucentral.co.tz kwa kuonyesha moyo wa kuwajali wasanii, lakini kwangu ni deni kwa mwaka huu wa 2011, mara nyingi watu wakipata tuzo huwa ndiyo wakati wa kubweteka, kwangu nisingependa iwe hivyo nahitaji kufanya kazi zaidi ili niwe mshindi tena kwangu ni heshima kubwa sana, nasema asante” Amesema Ali Yakuti mshindi wa uandishi wa mswaada.

“Tunawashukru waandaaji wa tuzo hizi kwa kweli mwaka huu umekuwa mzuri kwangu pamoja na kampuni yangu, tunawashukru sana tena na tena mtandao huu wa filamucentral.co.tz kwa kutukumbuka na kutujali”
Kanumba akiwa na tuzo zake alizoshinda.

0 comments:

Post a Comment