SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, January 20, 2011

TALKING ABOUT BROTHERHOOD… 
Mara kwa mara tumeshawahi kuongelea jinsi ambavyo watoto kutoka familia moja wanavyoweza kuchagua kufanya kazi au ajira zinazoshabihiana.Tumewahi kuongelea wanamuziki kupata watoto ambao nao huja kuwa wanamuziki. Familia ya Mzee Zorro na wanae Banana na Maunda ni mfano mzuri.Tumeshawahi kuongelea wanasiasa kupata watoto ambao huja kurithi “uanasiasa”. Mifano ni mingi ukiwemo wa Rais wetu,JK kuwa na mtoto mwanasiasa(Ridhiwani).
Mara chache tumeongelea watoto wa familia moja,kujishughulisha na jambo moja au mambo yanayokwenda sambamba bila kufuata moja kwa moja walichokuwa wakikifanya wazazi wao.Kwa bahati nzuri,nchini kwetu tunayo mifano kadhaa.Leo ninazo familia mbili au brothers kutoka familia mbili. Vijana wa Mzee Kilosa na kutoka kwa Mzee Michuzi.Nadhani utakubaliana na mimi nikisema kwamba hii ni mifano miwili mizuri ya “brotherhood”.Kupendana na kupeana support ya kila hali.Unayo mifano mingine ya brotherhood au sisterhood ambayo tunaweza kusema ni mifano ya kuigwa? Tutumie nasi tutaiweka hewani. Kwa leo,lemme say Big Up to Kilosa Brothers and Michuzi Brothers!
Kutoka kushoto ni DJ Bon Luv,DJ Mackay na DJ Venture. Hawa ni brothers kutoka familia moja ambao wote ni DJs.They are very good at what they do.
Kutoka kushoto; Muhidin Issa Michuzi, Othman Michuzi na Ahmad Michuzi(MichuziJr). Wakiongozwa na M.Issa Michuzi, hawa wote ni wapiga picha wazuri na pia Bloggers. Mfano mzuri wa picha ni hiyo ya juu ya kina Kilosa ambayo imepigwa na Othman Michuzi.
www.bongocelebrity.com

0 comments:

Post a Comment