SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, July 5, 2010

Muasi akana kumpa Charles Taylor almasi
Aliyekuwa Rais wa Liberia Charles Taylor
Aliyekuwa muasi kutoka Sierra Leone amekana kumpa aliyekuwa Rais wa Liberia Charles Taylor "almasi haramu zinazotumika kugharamia vita" katika kesi ya uhalifu wa kivita.
Issa Sesay, anayetumikia kifungo cha miaka 52 gerezani, amesema Bw Taylor hakuwa kiongozi wa kundi la waasi la Revolutionary United Front (RUF) wakati wa vita.
Bw Taylor anatuhumiwa kutumia almasi kuchochea ghasia huko Sierra leone zilizosababisha vifo vya maelfu ya watu.
Amekana mashtaka 11 yanayomkabili.
Mahakama ya uhalifu wa kivita huko the Hague inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imetumia zaidi ya miaka miwili kusikiliza kesi hiyo, Bw Taylor mwenyewe akiwa amesimamishwa kizimbani kwa miezi saba katika kipindi hicho.
Sesay, mwenye umri wa miaka 40, alihukumiwa Octoba 2009 na mahakama hiyo hiyo maalum, iliyoundwa mahsusi kuwashughulikia washukiwa wa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Mauaji na ubakaji
Bw Taylor, mwenye umri wa miaka 62, anashukiwa kuuza almasi na kununua silaha kwa ajili ya waasi wa RUF wa Sierra leone, waliokuwa wakijulikana sana kwa kukata mikono na miguu ya raia wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya mwaka 1991-2001.
Maelfu ya watu walifariki dunia katika mgogoro huo baina ya nchi mbili za Sierra Leone na Liberia.
Sesay, shahidi muhimu kutoa ushahidi kwa utetezi wa Bw Taylor, amesema hakuwahi kumpa Bw Taylor madini.
Ameiambia mahakama, " Hapana, sikumbuki kumgawia almasi Bw Charles Taylor."
Amekana pia kupokea silaha au risasi kutoka kwa Bw Taylor, na kwamba mara yake ya kwanza kumwona ni mwezi Mei 2000.
Sesay, amekiri kuwa baadhi ya makomando wa waasi walihusika na mauaji na ubakaji wakati wa mgogoro huo, na ukataji wa viungo ulitokea kweli.
Amesema, lakini haikuwa sera ya kundi hilo la waasi kufanya hivyo.

0 comments:

Post a Comment