SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, May 20, 2010

Maaskofu wa Ubelgiji waomba msamaha kwa wahanga walionajisiwa


Sample ImageMaaskofu wa Makanisa ya Ubelgiji leo wameomba msamaha kwa wahanga wote wa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia walivyofanyiwa na baadhi ya maaskofu kutokanchi mbalimbali duniani. Taarifa iliyotolewa na maaskofu hao imeeleza kuwa, wanawaomba radhi wahanga wote ambao walidhalilishwa kijinsia hivi karibuni na kundi la maaskofu waliopotoka katikanchi mbalimbali ulimwenguni. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, jukumu kubwa la maaskofu ni kudhamini usalama wa watoto, na kutaka tabaka hilo la watoto lihifadhiwe duniani kote. Baada ya kufichuliwa kashfa ya Maaskofu huko Austria, Ujerumani, Ireland na Marekani ya kuwanajisi watoto wa nchi hizo, Kanisa la Ubelgiji mwezi uliopita lilitaka maaskofu wote waliokumbwa na kukiri kutenda vitendo hivyo vichafu wanga'atuke katika uongozi wa kidini. Miaka 25 iliyopita Askofu mmoja wa mji wa Bruges alikuwa ni askofu wa kwanza wa Kikatoliki nchini Ubelgiji kuamua kujitoa kwenye uongozi wa kiroho baada ya kukumbwa na kashfa ya kuwanajisi watoto.
Kiswahili Radio.

0 comments:

Post a Comment