SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, July 6, 2014

benki ya NBC yafuturisha wateja wake jijini Dar

Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal (wa pili kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NBC Tanzania, Dk. Mussa Assad (wa pili kushoto) wakichukua mlo wa futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Mizinga Melu (wa pili kushoto) Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Mwinda Kiula Mfugale (kushoto), wafanyakazi na wateja wa benki hiyo wakijumuika pamoja katika hafla ya futari iliyoandaliwa na NBC kwa wateja wake jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wateja wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) wakijumuika katika futari iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Mizinga Melu ( kushoto) akiwaongoza baadhi ya wateja wa benki hiyo kushiriki futari waliyowaandalia jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuturu katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya NBC ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwajali na kuwa karibu wateja wao.
Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal (kushoto) akipokewa na Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC Tanzania, William Kallaghe na Mwenyekiti wa Bodi ya NBC, Dk. Mussa Assad (kulia) alipoalikwa kama mgeni rasmi katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment