SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, March 3, 2014

Mtangazaji wa Channel 10 Salumu Mkambala Apata Ajali

 Mtangazaji wa Channel 10, Salum Mkambala, akipelekwa Theatre katika Hospitali ya Tumbi, Kibaha, Pwani.
Msanii wa kundi la Mizengwe, Hemed Maliyaga (wa kwanza kulia) akisaidiana na ndugu pamoja na mke wa Mkambala (wa tatu kushoto) kumpeleka mgonjwa…

 ...Mkambala akiingizwa Theatre.
--

HALI ya Mtangazaji wa Channel 10, Salumu Mkambala aliyepata ajali jana alfajiri kwa kugongana na lori akiwa safarini kuelekea Morogoro inaendelea vizuri katika Hospitali ya Tumbi, Kibaha mkoani Pwani.

Akizungumza na mwandishi wetu hospitalini hapo, mdogo wa mtangazaji huyo, Ramadhani Mkambala alisema kaka yake alikuwa akielekea Morogoro na alipofika maeneo ya Vigwaza aligongana na lori alfajiri ya jana saa 10. 30 akiwa yeye na mtu mmoja aliyempa lifti.

Hata hivyo, chanzo cha ajali hiyo kilitajwa na Ramadhani kuwa ni kutokana na barabara ya eneo hilo kuwa na mashimo mengi hali iliyosababisha gari la kaka yake kuhama upande wake na kulivamia lori.PICHA,VIDEO NA HABARI: DEOGRATIUS MONGELA-GPL

0 comments:

Post a Comment