Mwemyekiti
wa Taasisi ya Catherine Foundation ya mjini Arusha ambaye pia ni Mbunge
wa Viti Maalum, Catherine Magige (kushoto) akikabidhi masaada wa unga
wa sembe kwaajili ya uji wa wanafunzi shule ya msingi Levolosi. Wanao
pokea ni Mwenyekiti Kamati ya Shule, Edward Ngomuo (kulia) Mwalimu Mkuu
Shule ya Luvolosi, Elisante Kaaya na Mwalimu wa Chakula shuleni hapo,
Frida Mallya.
*********
JAMII
imetakiwa kuwa na moyo wa kujitolea na kusaidia makundi mbalimbali yenye
uhitaji katika jamii hasa wanawake na watoto ili kujenga taifda lenye
matumaini na amani.
Hayo
yamesemwa jana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Catherine Foundation, ya
jijini Arusha, Catherine Magige wakati akikabidhi msaada wa unga wa
sembe na sukari kwaajili ya kuwapikia uji wanafunzi zaidi ya elfu moja
katika shule ya Msingi Levolosi ya mjini hapa kwa muda wa mwezi mmoja.
Magige
ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM) mkoa wa Arusha, amesema
kila mtu anapswa kujipima kwenye mizani ya ubinadamu, kujitafakari na
pia kujiuliza maswali magumu kwenye nafsi yake, kwamba, katika kipindi
kifupi cha uhai wake, ameacha nyuma matunda ya aina gani.
“Tunapaswa
tusambaze mbegu za matunda ya amani na upendo na si mbegu za
machafuko…kwani ndio mbegu ambazo sote tunapaswa kuzisambaza na
kuzipanda ili kujenga taifa lenye matumaini na amani,”alisema Magige.
Ni
ukweli usio pingika kuwa watoto wetu hawa tusipo wawezesha kupata elimu
sasa basi tutakuwa tumejingeneneazea wenyewe taifa la watu mbumbumbu na
wasio na ujuzi wa kufanya jambo lolote jema na matokeo yake wataishia
katika magenge ya uhalifu na watumiaji wa madawa ya kulevya.
Magige
amesema ili watoto wafanye vizuri darasani wanahitaji kushiba na si
familia zote zinamudu kuwapa chakula watoto wao kabla ya kwenda shule
hivyo taasisi yake ya Catherine Foundation imeona ichangie kulisha
watoto hao kwa mwezi mmoja.
“Sisi
kama wazazi hatuna budi kusaidia wazazi wengine ambao wanania njema na
watoto walio wazaa isipokuwa uwezo ndio unawakwamisha katika kutimiza
malengo yao ya kuwasaidia watoto wao katika elimu,” alisema Magige.
Aidha
amesema utaratibu wa kuwapa watoto chakula shule utaongeza kiwango cha
usikivu wa wanafunzi darasani na kuongeza ufaulu huku ukupunguza tatizo
la utoro mashuleni ambalo limekithiri katika shule nyingi nchini.
“Kufanya
hivi situ watoto watakuwa wasikivu darasani bali hata kuchangia kwa
kiwango cha ufaulu darasani na ni wazi kuwa hata mahudhurio yataongezeka
shuleni hapa,” alisema Magige.
Pia
amewataka wanafunzi wanafunzi kukazania masomo yao darasani, kudumisha
nidhami mingoni mwao huku akiwataka walimu kutimiza wajibu wao ipasavyo
kwa kuwapa elimu bora na malezi stahiki watoto hao na maadili mema.
Mapema
katika hotuma yake Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Levolosi, Elisante
Kaaya alisema shule hiyo ina wanafunzi 1,029 na gharama za kuwalisha kwa
mwaka zinakadiriwa kuwa zaidi ya Sh Milioni 10.
Aidha
Mwalimu Kaaya alisema kuwa ili kufanya zoezi hilo la kuwapa uji au
chakula wanafunzu linaendelea wameazimia kuwashirikisha wazazi na wadau
wengine wa elimu ili uwe endelevu na wenye kuleta tija.
Ofisa wa Catherine Foundation Lucy Bongole akizungumza jambo kabla ya makabidhiano kuanza.
Mwalimu
Mkuu wa shule ya Msingi Levolosi, Elisante Kaaya akitoa maelezo ya
shule hiyo na mpango wa kuwapa uju wanafunzi wanafunzi 1,029 na gharama
za kuwalisha kwa mwaka zinakadiriwa kuwa zaidi ya Sh Milioni 10.
Juice zikigawiwa kwa wanafunzi.
Mwenyekiti wa Shule ya Msdingi Levolosi ya jijini Arusha, Edward Ngomuo akisema neno.
Mwenyekiti wa Catherine Foundation na Mbunge wa viti Maalum Arusha, Catherine Magige akigawa juice kwa wanafunzi.
Mwenyekiti wa Catherine Foundation na Mbunge wa viti Maalum Arusha, Catherine Magige akizungumza.
Mwemyekiti
wa Taasisi ya Catherine Foundation ya mjini Arusha ambaye pia ni Mbunge
wa Viti Maalum, Catherine Magige (wapili kushoto) akimuweka katika kiti
maalum cha magurudumu, motto mlemavu Hassan Ramadhani (10) mkazi wa
Luvolosi mjini Arusha jana. Wanaoshuhudia ni mama mzazi wa motto huyo,
Hadija Hassan na Mwalimu Mkuu Elisante Kaaya wa Shule ya Msingi
Luvolosi.
Mwemyekiti
wa Taasisi ya Catherine Foundation ya mjini Arusha ambaye pia ni Mbunge
wa Viti Maalum, Catherine Magige (kushoto) akikabidhi masaada wa unga
wa sembe kwaajili ya uji wa wanafunzi shule ya msingi Luvolosi ya mjini
Arusha jana. Anaeshuhudia ni Mwalimu Mkuu Elisante Kaaya.
Wazazi na walimu wakipokea unga na sukari
wanafunzi nao wakipokea
Wawakilishi wa wazazi wakipokea msaada huo.
Mwalimu wa Chakula shuleni hapo, Frida Mallya akitoa neno la shukrani kwa taasisi ya Catherine Foundation.
Mwenyekiti wa Catherine Foundation, Catherine Magige akiagana na wanafunzi.
0 comments:
Post a Comment